Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w15 1/6 uku. 6-7
  • Sayansi Iko na Mipaka

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Sayansi Iko na Mipaka
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Sayansi na Maisha Yako
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
w15 1/6 uku. 6-7
Mwanasayansi katika chumba cha uchunguzi

HABARI KUBWA SAYANSI IMEKAMATA NAFASI YA BIBLIA?

Sayansi Iko na Mipaka

Hivi karibuni, vitabu vyenye kufasiria mawazo ya watu wenye hawaamini Mungu viliandikwa. Watu wengi wamependezwa na vitabu hivyo na vimetokeza ubishi sana. Kuhusu jambo hilo, David Eagleman, mwanasayansi mwenye kujifunza mambo ya ubongo aliandika hivi: “Watu fulani wenye walivisoma . . . wanawaza kama wanasayansi wanajua kila kitu.” Kisha aliongezea hivi: “Wanasayansi wazuri wanakubali mawazo ya watu wengine, na katika kazi yao wanatazamia kuvumbua mambo mapya.”

Mwanasayansi mwenye kujifunza vitu vyenye kuwa katika anga anatumia teleskope

Tangu zamani, wanasayansi wenye uwezo wamefanya maendeleo sana katika kutafuta majibu ya maulizo magumu sana juu ya ulimwengu. Lakini wengine wamefanya makosa makubwa katika uchunguzi wao. Isaac Newton ni mumoja kati ya wanasayansi wakubwa sana wenye wameishi. Alionyesha namna nguvu za uvutano zinafanya sayari, nyota, na vikundi vya nyota vikuwe katika ulimwengu mumoja. Alianzisha hesabu fulani zenye zinatumiwa leo ili kutengeneza ordinatere, kusafiri katika anga, na zinatumiwa katika fizikia ya nyukilia. Lakini Newton alifanya pia sayansi ya uongo yenye kutumia uchawi na kuangalia nyota ili kugeuza chuma kuwa zahabu.

Miaka zaidi ya 1500 mbele ya Newton, Ptolemy, mwanasayansi Mugiriki mwenye kujifunza vitu vyenye kuwa katika anga, alichunguza anga kwa kutumia macho yake tu. Alivumbua sayari katika anga la usiku na alikuwa na uwezo mukubwa wa kuchapa karte. Lakini aliamini kama dunia iko katikati ya ulimwengu. Carl Sagan, mwanasayansi mwengine, aliandika hivi juu ya Ptolemy: “Kwa miaka 1500 watu waliamini mafundisho yake kuwa dunia iko katikati ya ulimwengu, na hilo linaonyesha kama hata mutu mwenye akili nyingi anaweza kudanganyika sana.”

Mwanasayansi mwenye kusoma Biblia

Leo wanasayansi wanapambana pia na magumu hayo. Kuna siku wataweza kufasiria kila kitu juu ya ulimwengu? Ni muzuri kukubali kama sayansi imeendelea sana na imetuletea faida, lakini inafaa pia kujua kama sayansi iko na mipaka. Mwanasayansi Paul Davies alisema hivi: “Haiwezekane kupata mafasirio kamili na yenye kupatana juu ya kila kitu katika ulimwengu.” Maneno hayo yanaonyesha kweli hii yenye hakuna mutu anaweza kupinga: Wanadamu hawawezi kuelewa kila kitu katika ulimwengu. Kwa hiyo, wakati watu wanasema kuwa sayansi iko na uwezo wa kufasiria kila kitu, ni muzuri kuchunguza mbele ya kukubali jambo hilo.

Ni wazi kuwa Biblia inatutimizia mambo yenye sayansi haiwezi kutimiza

Biblia inazungumuzia maajabu ya ulimwengu. Inasema hivi: “Tazama vitu hivi ni kama kandokando tu ya njia [za Mungu]; na tunasikia manongono [maneno] yaliyo madogo sana katika habari zake!” (Ayubu 26:14, La Sainte Bible en swahili de la R.D. Congo) Kuna mambo mengi sana yenye wanadamu hawana uwezo wa kujua ao kuelewa. Kwa kweli, maneno haya yenye mutume Paulo aliandika kumepita miaka 2000 hivi yangali ya kweli: “Lo! Jinsi kilivyo kina [ukubwa] cha utajiri wa Mungu na hekima na ujuzi! Jinsi hukumu zake zisivyochunguzika na njia zake zisivyotafutika!”—Waroma 11:33.

Muongozo Wenye Sayansi Haiwezi Kutoa

Hata kama sayansi inatusaidia kujua ulimwengu, ni Biblia ndiyo inatutolea kanuni na muongozo wenye kutusaidia kuishi kwa amani na wengine, na kuwa na maisha yenye furaha. Fikiria mifano hii.

  • Mukono wenye kuonyesha alama ya kukataza

    Kuzuia Matendo ya Kuumiza Wengine

    Uheshimie uzima

    “Usiue.”—Kutoka 20:13.

    ‘Kila mutu anayemuchukia ndugu yake ni muuaji.’—1 Yohana 3:15.

    Uishi kwa amani na wengine

    “Geuka kutoka katika yaliyo mabaya, na kufanya yaliyo mema; utafute amani, na kuifuatia.”—Zaburi 34:14.

    ‘Mbegu ya tunda la uadilifu inapandwa chini ya hali zenye amani kwa wale wanaofanya amani.’—Yakobo 3:18.

    Uepuke jeuri

    ‘Yehova anachunguza muadilifu na pia muovu, na mutu yeyote anayependa jeuri nafsi Yake hakika inamuchukia.’—Zaburi 11:5.

    ‘Usimuonee wivu mutu mwenye jeuri, wala kuchagua yoyote kati ya njia zake. Kwa maana mutu mwenye hila [mujanja] ni chukizo kwa Yehova.’—Methali 3:31, 32.

  • Familia

    Furaha ya Familia

    Utii wazazi wako

    ‘Watoto, mutii wazazi wenu katika muungano na Bwana, kwa maana hilo ni jambo la uadilifu [haki]. Heshimu baba yako na mama yako; ambayo ndiyo amri ya kwanza yenye ahadi: Ili mambo yakuendee vema nawe ukae muda murefu duniani.’—Waefeso 6:1-3.

    Ufundishe muzuri watoto wako

    ‘Musiwe mukiwakasirisha watoto wenu, bali [lakini] muendelee kuwalea katika nizamu na muongozo wa akilini wa Yehova.’—Waefeso 6:4.

    ‘Musiwe mukiwakasirisha watoto wenu, ili wasivunjike moyo.’—Wakolosai 3:21.

    Umupende na umuheshimie bibi ao bwana yako

    ‘Kila mutu mumoja-mumoja kati yenu na amupende hivyo muke [bibi] wake kama vile anavyojipenda mwenyewe; kwa upande mwingine, muke anapaswa kumuheshimu sana mume [bwana] wake.’—Waefeso 5:33.

  • Muti

    Kulinda dunia

    Biblia ilisema hivi juu ya Waisraeli wenye zamani walikuwa wanaharibisha dunia: ‘Inchi imechafuliwa chini ya wakaaji wake . . . Wakaaji wake wamehesabiwa hatia [kosa].’ (Isaya 24:5, 6) Mungu ataazibu watu wenye kuharibisha dunia bila sababu. ‘Atawaharibu wale wanaoiharibu dunia.’ (Ufunuo 11:18) Hawatakosa kupata matokeo mabaya ya matendo yao.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine