Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w15 1/7 uku. 3
  • Kila Mahali Kuna Mahangaiko!

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kila Mahali Kuna Mahangaiko!
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Mahangaiko Juu ya Hatari
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Umutupie Yehova Mahangaiko Yako Yote
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2016
  • Mahangaiko Juu ya Familia
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Mahangaiko
    Amuka!—2016
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
w15 1/7 uku. 3

HABARI KUBWA | NAMNA YA KUPIGANISHA MAHANGAIKO

Kila Mahali Kuna Mahangaiko!

“Nilienda kununua chakula lakini nilikuta biskuti tu, na bei yake ilikuwa imeongezeka sana! Siku yenye ilifuata, maduka yote hayakuwa na chakula.”—Paul, inchi ya Zimbabwe.

“Bwana yangu aliniikalisha na akaniambia atatuacha.Namna gani ningevumilia hali hiyo? Watoto wangu wangekuwa namna gani?”—Janet, inchi ya Amerika.

Wakati ninasikia kelele ya kuonya watu juu ya hatari, ninakimbia ili kujificha na ninalala chini wakati bombe zinapigwa. Saa nyingi kisha hapo, mikono yangu inaendelea kutetemeka.”—Alona, inchi ya Israeli.

Mwanaume mwenye kuhangaika kwa sababu ya vita, umaskini, magonjwa, na matatizo ya maisha

Tunaishi nyakati za mahangaiko, ‘nyakati za hatari zilizo ngumu kushugulika nazo.’ (2 Timotheo 3:1) Watu wengi wanasumbuka kwa sababu ya matatizo ya feza, kuvunjika kwa familia, vita, magonjwa hatari, na misiba ya asili ao misiba yenye kuletwa na wanadamu. Zaidi ya hayo, kila mutu iko na mahangaiko yake mwenyewe. Kwa mufano, mutu anaweza kujiuliza hivi: ‘Kivimba chenye nilivumbua kwenye mwili wangu kitageuka kuwa kansere?’ ‘Watoto wa watoto wangu watakomalia katika dunia ya namna gani?’

Mahangaiko yote haiko mubaya. Kwa kawaida tunakuwa na mahangaiko mbele ya kufanya mashindano, mbele ya kufanya onyesho, ao mbele ya kuulizwa maulizo na mutu mwenye atatupatia kazi. Na woga wenye kufaa wa hatari unatusaidia tusipatwe na mambo mabaya. Lakini mahangaiko yenye kupita mipaka ao ya kila mara yanaleta hatari. Uchunguzi mbalimbali wa hivi karibuni wenye ulifanywa juu ya watu wazima 68 000 ulionyesha kama hata mahangaiko madogo ya kila mara yanaweza kufanya mutu akufe mbio. Kwa hiyo, Yesu alikuwa na sababu ya muzuri ya kuuliza hivi: ‘Ni nani kati yenu kwa kuhangaika anaweza kuongeza kipimo cha mukono mumoja kwenye uhai wake?’ Kwa kweli, mahangaiko hayarefushe maisha ya mutu. Ndiyo maana Yesu alitoa shauri hili: ‘Muache kuhangaika.’ (Mathayo 6:25, 27) Lakini, namna gani mutu anaweza kuacha kuhangaika?

Mutu anaweza kuacha kuhangaika ikiwa anatenda kwa hekima, anakuwa na imani ya kweli kwa Mungu, na anakuwa na tumaini la kweli kwa ajili ya wakati unaokuja. Hata kama leo hatupambane na hali ngumu, tunaweza kupambana nazo wakati unaokuja. Kwa hiyo, tuone namna kufanya mambo hayo kulisaidia Paul, Janet, na Alona wapiganishe mahangaiko yao.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine