Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w15 1/9 uku. 7
  • Sababu Gani Tunahubiri?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Sababu Gani Tunahubiri?
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Musaada Zaidi Kwa Ajili Ya Familia
    Amuka!—2018
  • Tunaweza Kupata Wapi Majibu ya Maulizo ya Maana Sana Juu ya Maisha?
    Tunaweza Kupata Wapi Majibu ya Maulizo ya Maana Sana Juu ya Maisha?
  • Unaweza Kupata Musaada wa Kuelewa Biblia
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • ‘Muende Mufanye Wanafunzi Kutoka kwa Watu wa Mataifa Yote’
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2016
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
w15 1/9 uku. 7
Mashahidi wawili wa Yehova wanahubiri katika eneo ambamo watu wanaishi

HABARI KUBWA | MASHAHIDI WA YEHOVA NI NANI?

Sababu gani tunahubiri?

Pengine kitu chenye kutufanya tukuwe tofauti zaidi na watu wengine ni kazi yetu kubwa ya kuhubiri. Tunahubiri nyumba kwa nyumba, nafasi zenye kuwa na watu wengi, na kila nafasi watu wanapatikana. Sababu gani tunafanya hivyo?

Mashahidi wa Yehova wanahubiri ili kusifu Mungu na kujulisha wengine jina lake. (Waebrania 13:15) Tena, tunapenda kutii Kristo Yesu mwenye aliamuru hivi: ‘Muende mukafanye wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote, . . . na kuwafundisha kushika mambo yote ambayo nimewaamuru ninyi.’—Mathayo 28:19, 20.

Zaidi ya hilo, tunapenda majirani wetu. (Mathayo 22:39) Ni kweli, tunatambua kama watu wengi wako na dini zao na kama haiko kila mutu atakubali ujumbe wetu. Lakini, tunaona kama mafundisho ya Biblia ni yenye kuokoa uzima. Ndiyo sababu tunaendelea “bila kuacha kufundisha na kutangaza habari njema juu ya Kristo Yesu,” kama vile Wakristo wa kwanza walifanya.—Matendo 5:41, 42.

Antonio Cova Maduro, mutu mwenye kujifunza namna watu wanapangwa, aliandika juu ya “bidii Mashahidi wa Yehova wanaonyesha na magumu wanapata, na kufikia hata kuchoka sana. . . , ili maandishi matakatifu yafike katika maeneo ya mbali zaidi ya dunia.”—Gazeti El Universal, Venezuela

Watu wengi wenye kusoma vichapo vyetu hawako Mashahidi wa Yehova. Na mamilioni ya watu wenye tunafundisha Biblia, wako na dini zao. Lakini, wanafurahi kuona Mashahidi wa Yehova wanawatembelea.

Pengine unaweza kuwa na maulizo mengine juu ya Mashahidi wa Yehova. Tunakutia moyo utafute majibu kwa:

  • Kuuliza Shahidi mumoja wa Yehova.

  • Kufungua adresi yetu ya Internete www.jw.org.

  • Kufika kwenye mikutano, yetu.Hatuombe malipo na watu wote wanaweza kuingia.

Yesu anatuma wanafunzi wawili waende kuhubiri
Mulima wenye kufunikwa na seluji

Ili kupata habari zingine juu ya Mashahidi wa Yehova, angalia video yenye kichwa Mashahidi wa Yehova—Tengenezo Linalohubiri Habari Njema, kwenye adresi yetu ya Internete www.jw.org. (Fungua kichwa MACHAPISHO > VIDEO)

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine