Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w15 1/11 uku. 16
  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Maulizo juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Kutakuwa Ufufuo!
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Ufufuo Ni Nini?
    Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
w15 1/11 uku. 16

MAULIZO JUU YA HABARI ZA BIBLIA YANAJIBIWA

Watu waliokufa wataishi tena?

Watu wanakaribisha wale wenye wanafufuliwa katika Paradiso

Kwa Kweli, Muumbaji wa uzima anaweza kurudisha Uzima

Yehova Mungu ndiye alianzisha uzima. (Zaburi 36:9) Hauone kama ni jambo lenye kupatana na akili kusema kama Mungu huyo huyo atawarudishia uzima watu waliokufa? Biblia inatuhakikishia kama atafanya hivyo wakati unaokuja. (Soma Matendo 24:15) Lakini sababu gani atafanya hivyo?

Wakati Muumbaji wetu aliumba mutu, alikusudia aishi milele katika dunia. (Mwanzo 1:31; 2:15-17) Angali na kusudi hilo kwa ajili ya wanadamu. Anahuzunika wakati anaona mambo yenye kutupata leo, ni kusema, maisha yenye kujaa taabu na yenye kuwa mafupi.—Soma Ayubu 14:1, 14, 15.

Watu wenye watafufuliwa wataishi wapi?

Mungu aliumba mutu ili aishi mbinguni? Hapana. Mungu aliumba malaika ili waishi mbinguni. Aliumba watu ili waishi duniani. (Mwanzo 1:28; Ayubu 38:4, 7) Ukiwa na wazo hilo katika akili, fikiria miujiza ya ufufuo yenye Yesu alifanya. Alifufua watu na waliishi tena hapa duniani. Vilevile, wengi kati ya watu wenye watafufuliwa wakati unaokuja, wataishi hapa duniani.—Soma Yohana 5:28, 29; 11:44.

Lakini, Mungu amechagua hesabu kidogo ya watu wenye watafufuliwa ili kuishi mbinguni, kwenye watakuwa na miili ya kiroho. (Luka 12:32; 1 Wakorintho 15:49, 50) Wale wenye watafufuliwa ili kuishi mbinguni watakuwa wafalme na watatawala pamoja na Kristo juu ya dunia.—Soma Ufunuo 5:9, 10.

Ili kupata habari zingine, soma sura ya 7 ya kitabu hiki, chenye kilichapishwa na Mashahidi wa Yehova

Unaweza pia kupata kitabu hiki kwenye adresi yetu ya Internete www.jw.org/swc

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine