Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • wp16 na. 1 uku. 11-14
  • Namna ya Kupiganisha Hali ya Kujisikia Kuwa Hauko Salama

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Namna ya Kupiganisha Hali ya Kujisikia Kuwa Hauko Salama
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2016
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • MAGUMU YA KUKOMAA KATIKA HALI YENYE HAINA USALAMA
  • MUNGU ANATUHANGAIKIA
  • MAMBO TATU YA KUFANYA ILI KUJISIKIA SALAMA ZAIDI
  • USALAMA KWA WATU WOTE
  • Hauko Peke Yako Juu Sikuzote Yehova Iko na Weye
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2021
  • Yehova Anakupenda Sana!
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2021
  • Biblia Inabadili Maisha
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Ufurahi juu ya Maendeleo Yako Mwenyewe!
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2021
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2016
wp16 na. 1 uku. 11-14

Namna ya Kupiganisha Hali ya Kujisikia Kuwa Hauko Salama

MUTOTO mwenye kutoka tu kuzaliwa ndiye mwenye kuonekana zaidi kuwa hana uwezo wowote. Wakati tulizaliwa, usalama wetu wote ulikuwa katika mikono ya wazazi wetu. Wakati tulijifunza kutembea, tuliona kama watu wenye walituzunguka walikuwa warefu kuliko sisi. Kama wazazi wetu hawakukuwa karibu, watu hao walituogopesha sana. Lakini tulijisikia kuwa salama wakati tulikamata mukono wa baba ao wa mama yetu.

Wakati tulikuwa watoto, wazazi wetu walituonyesha upendo na walitutia moyo, jambo hilo ndilo lilifanya tujisikie muzuri. Wakati tuliona kama wazazi wetu walitupenda, tulijisikia kuwa salama zaidi. Tulijisikia wenye uhakika zaidi na tulifanya maendeleo, wakati walituhakikishia kama tulikuwa tunafanya muzuri.

Wakati tulikomaa kidogo, marafiki wetu wa sana walitufanya pia tujisikie kuwa salama. Tulijisikia muzuri wakati tulikuwa nao, na walifanya tusiogope sana kwenye masomo.

Kwa kweli, mawazo hayo yanaonyesha namna maisha ya utoto yalikuwa. Vijana fulani hawapate marafiki wengi wa sana, na watoto wengi hawapate musaada kabisa kutoka kwa wazazi wao. Melissaa anasema hivi: “Wakati ninaona picha za watu wa familia wenye umoja wakifanya mambo pamoja, ninajiambia, ‘Mimi pia ningeishi hivyo wakati nilikuwa mutoto!’” Pengine na wewe unajisikia namna hiyo.

MAGUMU YA KUKOMAA KATIKA HALI YENYE HAINA USALAMA

Pengine haukujisikia salama wakati ulikuwa mutoto. Labda, haukuonyeshwa upendo mwingi na haukutiwa moyo sana. Inawezekana unakumbuka ugomvi wenye ulikuwa wa kawaida kati ya wazazi wako na namna jambo hilo lilifanya ndoa yao ivunjike, pengine uliwaza kimakosa kama ni wewe ulifanya jambo hilo litokee. Na jambo la mubaya zaidi, pengine baba ao mama yako alikuwa anakutukana ao kukupiga sana.

Mutoto mwenye kujisikia kuwa hana usalama anaweza kutenda namna gani? Hilo linafanya watoto fulani watumie dawa za kulewesha ao kunywa pombe sana katika miaka yao ya ujana. Wengine wanajiunga na vikundi vya watenda-mabaya ili wajisikie kama wanapendwa. Vijana wenye hawajisikie kuwa salama wanaanzisha haraka urafiki wa kimapenzi, ili kupendwa kutafuta na kuhangaikiwa. Lakini, kwa kawaida urafiki huo hauendelee kwa muda murefu, na wakati unavunjika, mara nyingi hilo linafanya wakose usalama zaidi.

Vijana wenye kukosa usalama ambao wanaepuka mambo hayo ya mubaya, nao pia wanaweza kukomaa na mawazo ya kujisikia kuwa hawako wa maana kabisa. Ana anaeleza hivi: “Nilifikia kuamini kama nilikuwa mutu wa bure, kwa sababu mama yangu alikuwa ananiambia jambo hilo tena na tena. Sikumbuke hata siku yenye alinipongeza ao kunionyesha upendo.”

Haiko tu namna watu walikomaa ndiyo inafanya wajisikie kuwa hawako salama. Tunaweza kujisikia kuwa hatuko salama kwa sababu ya kuvunjika kwa ndoa katika njia yenye kuumiza, magumu ya uzee, ao hata kwa sababu ya kuhangaikia sura yetu. Hata kama ni juu ya sababu gani, kujisikia kuwa hatuko salama kunaweza kutufanya tukose furaha na kunaweza kuharibisha urafiki wetu pamoja na wengine. Tunaweza kufanya nini ili kupiganisha hali hiyo?

MUNGU ANATUHANGAIKIA

Ni lazima tujue kama kuko musaada. Sisi wote tuko na mutu mwenye anaweza kutusaidia na mwenye anataka kutusaidia, ni kusema, Mungu mwenyewe.

Mungu alitoa ujumbe huu kupitia nabii Isaya: ‘Usiogope, kwa maana mimi ni Mungu wako. Nitakutia nguvu. Nitakusaidia kwelikweli. Nitakushika kwelikweli kwa mukono wangu wa kuume wa uadilifu [haki].’ (Isaya 41:10, 13) Ni jambo lenye kutuliza moyo kujua kama, kwa njia ya mufano, Mungu anapenda kutushika mukono! Hatuna sababu ya kuhangaika!

Biblia inazungumuzia waabudu wa Mungu wenye walihangaika lakini walijifunza kushika mukono wa Mungu. Hana, mama ya Samweli, alijisikia kuwa mutu wa bure, kwa sababu alikuwa tasa. Mara nyingi alizarauliwa kwa sababu ya jambo hilo. Hilo lilifanya apoteze hamu ya kula na alilia mara nyingi. (1 Samweli 1:6, 8) Lakini wakati alimuambia Mungu namna alikuwa anajisikia, hakuendelea kuwa na huzuni tena.—1 Samweli 1:18.

Daudi, muandikaji wa zaburi, alijisikia pia wakati fulani kuwa hakukuwa na usalama. Kwa miaka mingi, Mufalme Sauli alijaribu kumuwinda. Daudi aliponyoka mara nyingi wakati Sauli alitaka kumuua, na wakati fulani alijisikia kuwa anazama katika magumu yake. (Zaburi 55:3-5; 69:1) Hata kama alikuwa katika hali hiyo, aliandika hivi: ‘Nitajilaza na kulala usingizi, kwa maana wewe peke yako, Ee Yehova, unanifanya nikae kwa usalama.’—Zaburi 4:8.

Hana na Daudi, wote wawili, walimuambia Yehova namna walikuwa wanajisikia na waliona kama aliwasaidia. (Zaburi 55:22) Namna gani tunaweza kufanya kama wao leo?

MAMBO TATU YA KUFANYA ILI KUJISIKIA SALAMA ZAIDI

1. Ujifunze kutumainia Yehova kama Baba.

Yesu alituomba tumujue Baba yake, “Mungu wa pekee wa kweli.” (Yohana 17:3) Mutume Paulo anatuhakikishia kama ‘haiko mbali sana na kila mumoja wetu.’ (Matendo 17:27) Yakobo aliandika hivi: ‘Mumukaribie Mungu, naye atawakaribia ninyi.’—Yakobo 4:8.

Kujua kama tuko na Baba wa mbinguni mwenye anatupenda na mwenye anatuhangaikia, ni jambo la maana sana ili kupiganisha mahangaiko. Kwa kweli, inaomba wakati ili kuwa na tumaini hilo, lakini watu wengi wamevumbua kama kufanya hivyo kunasaidia kabisa. Caroline anasema hivi: “Wakati nilianza kumuona Yehova kama Baba yangu, nilifikia kupata mutu mwenye ningeweza kuambia namna nilijisikia katika moyo. Jambo hilo lilinituliza sana!”

Rachel anakumbuka hivi: “Yehova ndiye alinisaidia kujisikia salama wakati nilibakia mimi peke bila wazazi. Ningeweza kuzungumuza naye na kumuomba musaada. Na alinisaidia.”b

2. Utafute familia ya kiroho.

Yesu alifundisha wanafunzi wake waonane kuwa ndugu na dada. Aliwaambia hivi: ‘Ninyi wote ni ndugu.’ (Mathayo 23:8) Alipenda wanafunzi wake wa kweli wapendane kati yao na wafanyize familia kubwa ya kiroho.—Mathayo 12:48-50; Yohana 13:35.

Kwa kweli, makutaniko ya Mashahidi wa Yehova ni familia ya kweli ya kiroho kwenye watu wanapata furaha na kitulizo. (Waebrania 10:24, 25) Watu wengi wameona kama mikutano ya kutaniko ni kama dawa ya kupaka yenye kuponyesha vidonda vyao vya moyoni.

Eva anakumbuka hivi: “Katika kutaniko letu nilikuwa na rafiki wa kweli, mwenye alielewa magumu yangu. Alinisikiliza, alinisomea Biblia, na kusali pamoja na mimi. Alifanya yake yote ili nisijisikie kuwa peke yangu. Alinisaidia kuzungumuzia mambo kwa undani na kujiondolea muzigo. Kupitia musaada wake, nilianza kujisikia kuwa na usalama zaidi.” Rachel anaongezea hivi: “Nilipata ‘mama na baba’ katika kutaniko. Kwa kweli, walifanya nijisikie salama na mwenye kupendwa.”

3. Uonyeshe wengine upendo na wema.

Kuwaonyesha wengine upendo na wema kunasaidia kufanya marafiki wa kweli. Yesu alisema hivi: “Kuna furaha zaidi katika kutoa kuliko ilivyo katika kupokea.” (Matendo 20:35) Na kwa kweli, tutaona kama tukionyesha wengine upendo mwingi, watatuonyesha pia upendo mwingi. Yesu aliwaambia wanafunzi wake hivi: ‘Mukuwe na mazoea ya kuwapa watu, na watu watawapa ninyi’.—Luka 6:38.

Ikiwa tunaonyesha na kuonyeshwa upendo, tunajisikia kuwa salama zaidi. Kama vile Biblia inaonyesha, ‘upendo haushindwe kamwe.’ (1 Wakorintho 13:8) María anasema hivi: “Ninajua kama mawazo fulani ya mubaya yenye niko nayo juu yangu hayako ya kweli. Ninapiganisha mawazo hayo ya mubaya kwa kuwasaidia wengine na kwa kujisahau mimi mwenyewe. Sikuzote, ninasikia furaha wakati ninafanya jambo fulani kwa ajili ya wengine.”

USALAMA KWA WATU WOTE

Mambo yenye tunataja hapo juu haiko ‘dawa ya muujiza’ yenye kuleta palepale kitulizo cha kuendelea. Lakini, yanaweza kusaidia sana. Caroline anasema hivi: “Ningali ninajisikia kuwa mwenye kukosa usalama. Lakini sasa ninajiona kuwa wa maana. Ninajua kama Mungu ananihangaikia, na niko na marafiki wengi wa sana wenye kunifanya pia nijisikie salama.” Rachel naye anajisikia hivyo. Anasema hivi: “Mara kwa mara, ninasikia huzuni nyingi. Lakini niko na ndugu na dada wa kiroho wenye ninaweza kuomba mashauri na wenye wananisaidia kuwa na mawazo ya muzuri. Na zaidi ya hilo, niko na Baba wa mbinguni mwenye ninazungumuza naye kila siku. Mambo hayo yananisaidia sana.”

Biblia inazungumuzia dunia mupya na katika dunia hiyo, watu wote watajisikia kuwa salama

Tena, kuko jambo lenye litamaliza milele hali ya kukosa usalama. Biblia inazungumuzia dunia mupya na katika dunia hiyo, watu wote watajisikia kuwa salama. Neno la Mungu linaahidi hivi: ‘Wataketi [watakaa], kila mutu chini ya muzabibu wake na chini ya mutini wake, wala hakutakuwa na mutu yeyote anayewatetemesha.’ (Mika 4:4) Wakati huo hakuna mutu atatukosesha usalama, ao kutufanya mubaya. Hata mambo ya kuhuzunisha sana ya wakati uliopita “hayataingia moyoni.” (Isaya 65:17, 25) Mungu na Kristo Yesu, Mwana wake, wataleta “uadilifu [haki] wa kweli.” Jambo hilo litatokeza ‘utulivu na usalama mupaka wakati usio na kipimo.’—Isaya 32:17.

a Majina yote yamebadilishwa.

b Mashahidi wa Yehova wanajifunza Biblia bila kulipa pamoja na watu wenye wanapenda kumukaribia Mungu zaidi.

Walipambana na Hali ya Kukosa Usalama

“Wakati hasira ilikuwa inamupanda baba yangu mulevi, sura yake ilibadilika. Alikuwa anageuka kama imbwa wa pori mwenye kutoa meno yake inje mbele ya kushambulia munyama fulani bila huruma. Na nilikuwa kama mwana-kondoo mwenye kuogopa, nilikuwa ninatetemeka na kujificha, na kutumainia kama hataniona. Niliishi katika hali hiyo ya kuogopesha karibu kila siku.”—Caroline anakumbuka maisha yake ya utoto.

“Nilijisikia kuwa singeweza kutumainia mutu yeyote. Nilikuwa kama mutu mwenye kupotea juu ya mulima na nililalamika ili kupata musaada, lakini sikupata mutu yeyote wa kunisikia, ao mutu wa kundiongoza katika nafasi salama.”—Eva, mwanamuke mwenye ndoa yake imevunjika hivi karibuni.

“Mara nyingi, baba yangu alikuwa ananifokea, ‘Uko mutu mubaya. Hakuna mutu atakupendaka!’ Kwa miaka mingi, nilijaribu kujihakikishia kama niko mutu muzuri na kama wengine wananipenda kabisa. Nilijisikia kama mutoto wa imbwa mwenye kutia mukia katikati ya miguu, mwenye kutafuta sikuzote mutu wa kumugusa-gusa kwenye manyoya lakini bila kumupata hata siku moja.”—Mark, mwenye baba yake alikuwa anashushia heshima.

“Wakati fulani ninaangalia mwanamuke wa sura ya muzuri na ninamulinganisha na ua la muzuri sana la okidi lenye watu wanaweza kupenda kuwa nalo katika nyumba zao. Lakini mimi niko kama mumea usiofaa wenye hauwezi kupendeza mutu yeyote.”—María, kijana mwanamuke mwenye kupambana na mawazo ya kujiona kama haiko wa maana.

“Wakati nilikuwa na miaka 12 tu, wazazi wangu walihamia katika inchi ingine na waliniachia wadogo wangu wawili wanawake ili niwachunge. Nilijisikia kuwa peke yangu. Nilipenda mutu fulani anihangaikie na kuniambia kama nilikuwa ninafanya mambo muzuri. Lakini, nilijisikia kama vile mutu mwenye kupotea katika pori kubwa na lenye giza. Hata kama nilikuwa katika pori hilo siku kwa siku, nilipenda kupata njia ya kutoka. Nilipenda nijisikie kuwa salama na mwenye furaha.”—Rachel, mutoto mwanamuke mwenye wazazi wake wanatumikia katika inchi ya kigeni.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine