Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w16 Mwezi wa 12 uku. 29-31
  • Tabia-Pole—Njia Yenye Kuonyesha Hekima

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Tabia-Pole—Njia Yenye Kuonyesha Hekima
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2016
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • HEKIMA YENYE KUTOKANA NA ROHO YA TABIA-POLE
  • Upole​—Unatuletea Faida Gani?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
  • Upole Haiko Uzaifu, Ni Nguvu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2023
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2016
w16 Mwezi wa 12 uku. 29-31
Mutu mumoja mwenye kuwa na uzoefu wa kutunza watu wenye kuzeeka anazungumuza na mwanamuke mumoja mwenye kuwa na hasira

Tabia-Pole Njia Yenye Kuonyesha Hekima

Toñi, mwanamuke mumoja mwenye kuwa na uzoefu wa kutunza watu wenye kuzeeka alipiga hodi kwenye mulango, na mwanamuke mumoja mwenye kuwa na miaka 50 hivi alijibia. Mwanamuke huyo alimuchambua Toñi na kumufokea kwa sababu hakufika mbele ya wakati ili kutunza mama mwenye kuzeeka wa mwanamuke huyo. Toñi hakuchelewa kwenye kazi. Lakini, aliomba mwanamuke huyo musamaha kwa upole kwa sababu hawakuelewana.

SIKU ingine, mwanamuke huyo alitombokea tena Toñi. Alitenda namna gani? Alisema hivi: “Ilikuwa hali ngumu sana; hakukuwa na sababu ya kunitukana vile.” Hata hivyo, Toñi aliomba tena musamaha na kuambia mwanamuke huyo kama alielewa magumu yenye alikuwa nayo.

Ungekuwa Toñi, unafikiri wewe ungetenda namna gani? Ungejikaza kuonyesha tabia-pole? Ingekuwa vigumu kuzuia hasira yako? Kusema kweli, inaweza kuwa vigumu kuzuia hasira katika hali kama ile yenye kuzungumuziwa hapo juu. Wakati tuko na mahangaiko ao wakati watu wanatuchokoza, ni vigumu kabisa kuonyesha tabia-pole.

Lakini, Biblia inatia moyo Wakristo wakuwe na tabia-pole. Kwa kweli, Neno la Mungu linapatanisha sifa hiyo na kuwa na hekima. Yakobo anauliza hivi: ‘Ni nani aliye na hekima na mwenye uelewaji kati yenu? Na aonyeshe kutokana na mwenendo wake muzuri matendo yake kwa upole ulio wa hekima.’ (Yak. 3:13) Ni katika njia gani sifa ya tabia-pole inaonyesha hekima yenye kutoka juu? Na ni nini inaweza kutusaidia kukomalisha sifa hiyo yenye kumupendeza Mungu?

HEKIMA YENYE KUTOKANA NA ROHO YA TABIA-POLE

Tabia-pole inaweza kutuliza hasira. ‘Jibu, linapokuwa la upole, linageuza gazabu [hasira], lakini neno linaloumiza linafanya hasira ipande.’—Met. 15:1.

Kujibia kwa hasira kunaweza kufanya hali ya mubaya ikuwe ya mubaya zaidi kwa sababu hilo linaongeza mafuta kwenye moto. (Met. 26:21) Lakini, jibu lenye kutolewa kwa tabia-pole mara nyingi linatuliza. Linaweza hata kutuliza mutu mwenye kuwa mukali sana.

Toñi alijionea jambo hilo. Wakati aliona namna Toñi alimujibia kwa tabia-pole, mwanamuke huyo alianza kulia. Alimuelezea kama alikuwa anahangaika sana kwa sababu ya magumu yake mwenyewe na ya familia yake. Toñi alitoa ushahidi wa muzuri, na funzo la Biblia lilianzishwa; aliweza kufanya hivyo kwa sababu alionyesha sifa ya upole na roho ya kufanya amani.

Sifa ya tabia-pole inaweza kutuletea furaha. ‘Wenye furaha ni wale walio na tabia-pole, kwa kuwa watairiti dunia.’—Mt. 5:5.

Sababu gani wale wenye kuwa na tabia-pole wako na furaha? Watu wengi wenye walikuwa wakali zamani, wamekuwa na furaha sasa kwa sababu wanaonyesha sifa hiyo. Wamekuwa na maisha ya muzuri, na wanajua kama watakuwa na maisha ya muzuri zaidi wakati unaokuja. (Kol. 3:12) Adolfo, mwangalizi mumoja wa muzunguko katika inchi ya Uhispania, anakumbuka namna maisha yake yalikuwa mbele ajue kweli.

Adolfo anasema hivi: “Maisha yangu hayakukuwa na kusudi; nilikuwa na tabia ya kukasirika haraka sana; kwa hiyo, hata marafiki wangu fulani wanaume walikuwa wananiogopa kwa sababu ya matendo yangu yenye kiburi na jeuri. Mwishowe mambo yalibadilika. Katika pigano moja, niliumizwa vidonda sita kwa kunitoboa na kisu na damu ilinilitoka karibu kufa.”

Lakini sasa, kupitia maneno na mufano wake, Adolfo anafundisha wengine wakuwe na tabia-pole. Watu wengi wanajisikia huru kumukaribia na wanapendezwa na sifa zake za muzuri. Adolfo anasema kama yeye ni mwenye furaha kwa sababu ameweza kufanya mabadiliko. Na ni mwenye shukrani kwa Yehova kwa sababu amemusaidia kukomalisha sifa ya tabia-pole.

Tabia-pole inamufurahisha Yehova. ‘Ukuwe na hekima, mwanangu, na kuufanya moyo wangu ushangilie, ili nipate kumujibu anayenizihaki [anayenichokoza].’—Met. 27:11.

Kwa kweli, Yehova anachokozwa na adui wake mukubwa zaidi, ni kusema, Shetani. Mungu ana sababu zote za kuwa na hasira juu mambo yote ya mubaya yenye kusemwa kimakusudi juu yake, lakini Biblia inaonyesha kuwa Yehova “si mwepesi wa hasira.” (Kut. 34:6) Wakati tunajikaza kuiga sifa ya Mungu ya kutokuwa mwepesi wa hasira na upole wake, tunafuata njia ya hekima yenye kumupendeza sana Yehova.—Efe. 5:1.

Watu wa ulimwengu huu ni wakali kila mara. Tunaweza kukutana na watu “wenye kujidai [wenye kiburi], wenye majivuno, wakufuru, . . . wachongezi, wasiojizuia, wakali.” (2 Tim. 3:2, 3) Lakini, hilo haliwezi kuzuia Mukristo kukomalisha roho ya upole. Neno la Mungu linatukumbusha kama “hekima inayotoka juu ni . . . yenye kufanya amani, yenye usawaziko.” (Yak. 3:17) Wakati tunaonyesha roho ya kufanya amani na ya usawaziko, tunaonyesha wazi kama tumepata hekima yenye kutoka kwa Mungu. Hekima hiyo itatuchochea tujibie kwa upole wakati watu wanatuchokoza na itafanya tukaribie hata zaidi Chanzo cha hekima yenye haina mipaka, ni kusema, Yehova.

Namna ya Kukomalisha Sifa ya Tabia-Pole

Ikiwa mutu fulani anakutendea kwa ukali ao bila haki, ni nini inaweza kukusaidia kuzuia hasira yako na kutenda katika njia yenye kumufurahisha Yehova? Unaweza kufikiri sana juu ya kanuni hizi za maana sana.

  1. 1 EPUKA “ROHO YA ULIMWENGU.”—1 Kor. 2:12. Watu wengi wanaona upole kuwa ni uzaifu. Wanawaza kama ili mutu akuwe mwenye nguvu, anapaswa kuwa mwenye kukaza wengine na mukali. Mawazo hayo hayaonyeshe hekima kutoka juu, lakini yanaonyesha roho ya ulimwengu. Kwa kweli, Biblia inaonyesha wazi kama mutu mwenye kuwa na tabia-pole ana nguvu nyingi. ‘Kwa subira [uvumilivu] kiongozi anashawishiwa, na ulimi wa upole unaweza kuvunja mufupa.’—Met. 25:15.

    Maulizo ya kufikiria:

    Ninaona tabia-pole kuwa alama ya kuwa na nguvu ao uzaifu?

    Ninajikaza kuepuka “milipuko ya hasira [kukasirika haraka] na magomvi?” —Gal. 5:19, 20.

  2. 2 UKUWE NA WAKATI WA KUFIKIRI SANA. ‘Moyo wa muadilifu unatafakari ili kujibu, lakini kinywa cha waovu kinabubujika [kinasema-sema] mambo mabaya.’ (Met. 15:28) Ikiwa tunasema wakati tungali na hasira, tunaweza kusema-sema mambo yenye tutahuzunikia kisha wakati fulani. Lakini, ikiwa tunafikiri sana ao kuwaza mbele ya kusema, tutaweza kuchunguza mawazo yetu, kujibia kwa upole, na hilo litachochea wengine watutendee muzuri.

    Maulizo ya kufikiria:

    Kukasirika haraka kutaniletea matokeo gani?

    Ili kuendeleza amani, ninaweza kusamehe ikiwa wengine wananitendea bila haki?—Met. 19:11.

  3. 3 USALI KILA MARA. Usali ili upate roho takatifu, nguvu kubwa zaidi katika ulimwengu. (Lu. 11:13) Ukumbuke kama sifa ya upole na ya kujizuia ni sehemu za tunda la roho takatifu ya Mungu. Adolfo anakumbuka hivi: “Kuendelea kusali kwa Yehova kumenisaidia sana, zaidi sana wakati niko katika hali ngumu.” Vilevile, Yehova atajibia sala zetu zenye tunamutolea kwa moyo wote ili kumuomba roho takatifu ikiwa ‘tunadumu katika sala.’—Rom. 12:12.

    Maulizo ya kufikiria:

    Ninasali kwa Yehova kwa ukawaida ili achunguze moyo na nia yangu?

    Ninamuomba roho yake takatifu na hekima ili nitende katika njia yenye kumupendeza?—Zab. 139:23, 24; Yak. 1:5.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine