Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • wp17 na. 3 uku. 3
  • Namna Wapanda-Farasi Ine Wanakuhusu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Namna Wapanda-Farasi Ine Wanakuhusu
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2017
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Wale Wapanda-Farasi Ine Ni Nani?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2017
  • Utangulizi
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2017
  • Wale Wenye Kupanda Farasi Ine
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2019
  • Vita ya Ukraine Imefanya Chakula Ikosekane mu Dunia Yote
    Habari Zingine
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2017
wp17 na. 3 uku. 3
Mwendo wa farasi ine

HABARI KUBWA | WAPANDA-FARASI INE​—WANAKUHUSU NAMNA GANI?

Namna Wapanda-Farasi Ine Wanakuhusu

Farasi wanatokea haraka, na miguu yao inafanya makelele mengi! Picha ya farasi ine wenye nguvu na wale wenye kuwaongoza, inaonekana kuwa kweli katika akili, hivi kwamba inakuwa kama wanaruka kutoka katika kurasa za Biblia! Farasi wa kwanza ni wa rangi ya mweupe​—mwenye kuongoza farasi huyo ni mufalme mwenye utukufu ambaye ametoka tu kuvalishwa taji. Na nyuma yake kuna farasi wa rangi ya moto, na mwenye kuwa juu yake anaondoa amani katika dunia yote. Kisha kunakuja farasi wa tatu, mweusi kama giza, akiwa mwenye kubeba mupanda-farasi ambaye anakamata mizani (balance) wakati kunatangazwa ujumbe wa huzuni kuhusu ukosefu wa chakula cha musingi. Farasi wa ine ni wa rangi ya mubaya sana ya kijivu, na mwenye kuongoza farasi huyo ni Kifo chenyewe. Hiyo ni alama ya magonjwa na mapigo mengine yenye kuua. Na Kaburi, ni kusema, kaburi la ujumla la wanadamu wote, inafuata mupanda-farasi huyo kwa ukaribu, ikivuna uzima wa watu wengi sana!​—Ufunuo 6:1-8.

“Niliogopa sana wakati nilisoma kwa mara ya kwanza juu ya wale wapanda-farasi ine. Nilijisikia kama Siku ya Hukumu ilikuwa inakuja na kwa sababu sikuwa tayari, singeweza kuokoka.”​—Crystal.

“Nilivutiwa na wapanda-farasi mbalimbali wenye kuwa juu ya farasi wa rangi tofauti-tofauti. Kisha kupata maana ya maono hayo, nilielewa kabisa.”​—Ed.

Unajisikia kama Crystal wakati unasoma kuhusu wale wapanda-farasi ine wenye kuzungumuziwa katika Ufunuo? Ao unajisikia kama Ed? Ikuwe unajisikia kama Crystal ao Ed, habari kuhusu wapanda-farasi hao ni moja kati ya habari zenye kujulikana zaidi katika Ufunuo, kitabu cha mwisho cha Biblia. Ulijua kwamba kuelewa maono hayo kunaweza kukuletea faida? Namna gani? Mungu anaahidi kwamba unaweza kupata furaha ya kweli kwa kusoma na kujifunza mambo yenye kupatikana katika kitabu hicho cha unabii, na kwa kuishi kulingana nayo.​—Ufunuo 1:1-3.

Hata kama watu fulani wanaogopa maono kuhusu wapanda-farasi ine, ujue kwamba kusudi la maono hayo haiko kukuogopesha. Kusema kweli, mamilioni ya watu wameona kwamba maono hayo yametia imani yao nguvu na hata kuwapatia tumaini nzuri kwa ajili ya wakati wenye kuja. Wewe pia unaweza kujionea jambo hilo! Tafazali, soma habari yenye kufuata.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine