Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • wp18 na. 3 uku. 12
  • Ni Nani Anatuletea Mateso?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Ni Nani Anatuletea Mateso?
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2018
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Juu ya Nini Kuko Mateso Mingi Sana?
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Mambo Biblia Inasema Juu ya Mateso
    Amuka!—2015
  • Biblia Inasema Nini?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2017
  • Sababu Gani Mungu Anawaacha Watu Wateseke?
    Biblia Inafundisha Kabisa Nini?
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2018
wp18 na. 3 uku. 12
Watu wenye kutoa musaada wa kwanza wako mahali kwenye kulifanyika aksidenti ya motokari

Ni Nani Anatuletea Mateso?

Ikiwa haiko Mungu ndiye anatuletea mateso, ni nani anafanya watu wengi waishi katika njaa kubwa, umaskini wenye hauishe, vita kali, magonjwa hatari, na misiba ya asili? Neno la Mungu, Biblia, linaonyesha sababu tatu kubwa zenye zinafanya watu wateseke:

  1. Uchoyo, Pupa, na Chuki. “Mwanadamu ametawala mwanadamu mwenzake ili kumuumiza.” (Muhubiri 8:9) Mara nyingi watu wanateseka kwa sababu ya watu wenye hawakamilike, wachoyo, ao watu wakali.

  2. Wakati na Matukio Yenye Hayatazamiwe. Mara nyingi watu wanateseka “kwa sababu wakati na matukio yenye hayatazamiwe yanafikia wote.” (Muhubiri 9:11) Ni kusema, watu wako pa nafasi ya mubaya kwa wakati mubaya, aksidenti zinatokea, ao watu hawako waangalifu ao wanafanya makosa.

  3. Mutawala Muovu wa Ulimwengu. Biblia inaonyesha waziwazi sababu kubwa yenye inafanya wanadamu wateseke. Inasema hivi: “Ulimwengu muzima unakaa katika nguvu za ule muovu.” (1 Yohana 5:19) Ule “muovu” ni Shetani Ibilisi, kiumbe wa roho mwenye nguvu ambaye zamani alikuwa malaika wa Mungu lakini “hakusimama imara katika kweli.” (Yohana 8:44) Viumbe wengine walijiunga na Shetani na kumuasi Mungu ili kutimiza tamaa zao za uchoyo, na kwa hiyo wakajifanya kuwa pepo wachafu. (Mwanzo 6:1-5) Tangu uasi wao, Shetani na pepo wake wachafu wamechochea kwa njia mubaya sana mambo ya ulimwengu. Hilo limeonekana zaidi sana leo. Leo, Ibilisi iko na kasirani kali na “anapotosha dunia yote yenye kuikaliwa na watu,” na hilo limeleta “ole wa dunia.” (Ufunuo 12:9, 12) Kwa kweli, Shetani ni mutawala mukali sana. Anafurahi sana wakati watu wako wanateseka. Ni Shetani ndiye anafanya watu wateseke, haiko Mungu.

FIKIRIA JAMBO HILI: Ni mutu tu mwenye hana huruma na mubaya sana ndiye anaweza kufanya watu wenye hawana kosa wateseke. Lakini kuhusu Mungu, Biblia inasema hivi: “Mungu ni upendo.” (1 Yohana 4:8) Kwa sababu yeye ni upendo, “ni jambo lenye haliwezi kuwaziwa kwamba Mungu wa kweli atende uovu, na Mweza-Yote afanye makosa!”​—Yobu 34:10.

Hata hivyo, pengine unaweza kujiuliza, ‘Ni mupaka wakati gani Mungu Mweza-Yote ataacha Shetani aendelee kutawala kwa ukali?’ Kama vile tumekwisha kuona, Mungu anachukia sana mambo maovu na mateso yetu yanamuumiza sana. Zaidi ya hilo, Neno lake linatutia moyo hivi: “Mumutupie mahangaiko yenu yote, kwa sababu yeye anawahangaikia ninyi.” (1 Petro 5:7) Mungu anatupenda na iko na nguvu ya kuondoa mateso yote na ukosefu wa haki, kama vile tutaona katika habari yenye kufuata.a

a Ili kupata habari zaidi kuhusu juu ya nini kuko mateso mingi sana, ona somo ya 26 ya kitabu Furahia Maisha Milele! yenye kuchapishwa na Mashahidi wa Yehova na unaweza kuichukua bila kulipa ku www.jw.org.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine