Ni Nini Miradi Yetu Katika Kipindi cha Mapumziko ya Shule?
Tunapofikiria miezi ya Julai, Agosti na Septemba, tunafikiria, mipango ya kuchukua ili kuhudhuria kwenye kusanyiko la wilaya, na kwa miradi yetu: mapumziko yenye kuburudisha au ziara nzuri kwa wazazi au kwa marafiki. Angalieni vikumbusho fulani ambavyo vitatusaidia kutoa nafasi ya kwanza kwa kusudi la Ufalme huku tukipanga programu kwa ajili ya kipindi hicho.
◼ Tuchukue mipango kamili ili kuhudhuria kwenye kusanyiko la wilaya. Ili kuepuka tatizo lolote, tupange kimbele usafirishaji wetu na upangaji wetu mapema.
◼ Ikiwa tunakwenda katika mapumziko, tujitayarishe ili kuhudhuria kwenye mikutano ya kutaniko la mahali na kushiriki katika huduma. Tuangalie ili tutoe ripoti zetu za mahubiri; ikiwezekana, tuzitume kwa njia iliyo haraka zaidi na iliyo hakika, kwa mwandishi wa kutaniko letu.
◼ Ziara ya wazazi wasiokuwa katika ukweli itakuwa labda nafasi ya kutoa ushuhuda wa vivi hivi wenye matokeo. Tuwe waangalifu kuchukua Biblia yetu na vichapo vingi.
◼ Tungesema nini kuhusu kutoa usaidizi wetu kwa kutaniko la karibu nasi linalohitaji msaada ili kutembelea kikamilifu eneo lalo? Wazee au mwangalizi wa mzunguko wataweza kutufahamisha juu ya mahitaji yaliyopo katika mahali petu.
◼ Mapumziko ya shule ni nafasi bora kwa vijana kuongeza utendaji wao wa mahubiri. Vijana, je! mnaweza kuwa mapainia wasaidizi?
◼ Kwa wakati ulio nzuri na kwa siku ndefu zaidi, tutaona bila shaka kwamba tunapata matokeo bora ikiwa tunahubiri zaidi jioni, wakati watu walio wengi wanapopatikana makwao.
◼ Wazee wangepaswa hasa zaidi kuangalia ili kulinda programu nzuri ya utendaji wa kutaniko, kwa kuchukua mipango ili kwamba kazi zinazotolewa kwa wale watakaokwenda mapumzikoni zitimizwe na wengine.
Tukumbuke kwamba “mawazo ya wenye bidii huuelekea utajiri tu.” (Mit. 21:5) Tupange vizuri wakati wetu kwa jinsi tufaidike kikamilifu na nafasi za kutumikia theokrasi.