Tufuate Yesu Kwa Kuendelea
1 Katika kipindi fulani, Yesu alisema: “Ikiwa yeyote ataka kunifuata, na ajikane mwenyewe na kuchukua mti wake wa mateso na kunifuata kwa kuendelea.” (Mt. 16:24, Tafsiri ya Ulimwengu Mpya) Tunatamani hakika kuitikia vizuri kwa mwaliko wa Yesu. Tuone kile unamaanisha kwa kuchunguza kila msemwa.
2 “Na Ajikane Mwenyewe”: Kwa kuweka wakfu uhai wetu kwa Yehova, tunajikana wenyewe. Maana ya kwanza ya neno la Kigiriki linalotafsiriwa na ‘kukana’ ni “kusema hapana.” Hilo linamaanisha hivyo kwamba tunaachana kwa kujipendea na nia yetu ya kutaka makuu, tamaa zetu na starehe yetu kibinafsi, na pia na anasa zetu za kichoyo, tukiwa wenye kuazimia kumpendeza Yehova kwa umilele.—Rum. 14:8; 15:3.
3 “Kuchukua Mti Wake wa Mateso”: Kuishi kama Mkristo, ni kuishi kwa kuchukua mti wa mateso ambao ni utumishi unaotolewa kwa Yehova katika roho ya kujidhabihu. Mojawapo ya namna ya kuonyesha roho hiyo ni kujitoa katika huduma. Tangu mwanzoni mwa mwaka huu, wahubiri wengi walianzisha utumishi wa painia msaidizi. Ikiwa wewe ni kati yao, unaweza bila shaka kuhakikisha kwamba baraka zinazotokana na utumishi huo zinalipia kwa uwingi zaidi dhabihu zinazofanywa. Kwa wahubiri ambao ni vigumu kuanzisha utumishi huo mara nyingi wamepanga mambo yao ili kuhubiri zaidi. Ni kwa sababu hiyo makutaniko fulani yalisukuma mbele dakika fulani za mikutano yao kwa ajili ya mahubiri. Wakati wa kipwa unapofika, wahubiri wengi wanafaidika na wakati huo mzuri ili kuhubiri. Wamoja walipata matokeo bora, hasa wakati walipotaka kuhubiri ‘nyumba ya mwisho’ au kuhubiri ‘dakika chache za ziada.’
4 Kujiwekea miradi ya kibinafsi ni namna nyingine ya kuonyesha roho ya kujidhabihu. Kwa kupanga kwa makini programu na kwa kurekebisha matumizi yao ya wakati, wamoja walifikia kuwa mapainia wa kawaida. Wengine walifaulu kupanga mambo yao na kuwa tayari kutumikia Betheli au kama vile wamishonari. Wengine tena walikwenda kukaa katika eneo ambako uhitaji wa wahubiri wa Ufalme ni mkubwa.
5 “Kunifuata kwa Kuendelea”: Ingawa wanafunzi wa Yesu walipatwa na majaribu mengi, walipata kitia moyo katika juhudi na ustahimilivu aliokuwa akionyesha katika huduma yake. (Yn. 4:34) Walikuwa wakihisi roho yao ikifanywa upya kwa msaada wa kuwapo kwake na kwa ujumbe wake. Ni kwa sababu hiyo wale waliokuwa wakimfuata walikuwa wakihisi shangwe ya kweli. (Mt. 11:29) Vivyo hivyo, tutiane moyo wamoja kwa wengine kutimiza kwa ustahimilivu kazi ya maana inayohusu kuhubiri Ufalme na kufanya wanafunzi.
6 Basi sote na tuitikie vizuri mwaliko wa Yesu wa kuendelea kumfuata kwa kukomaza roho ya kujidhabihu! Hivyo, tutapata shangwe kubwa tangu sasa na tunaweza kutazamia baraka nyingi zaidi wakati ujao.