Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 7/97 uku. 1
  • “Fanya Yote Uwezayo Kabisa”

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • “Fanya Yote Uwezayo Kabisa”
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Ukuwe na Furaha Wakati Unafanya Yako Yote kwa Ajili ya Yehova
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2022
  • Unatimiza kwa Ukamili Utumishi Wako?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2019
  • Ujikaze Sana Kuingia Katika Pumuziko la Mungu
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2019
Huduma Yetu ya Ufalme—1997
km 7/97 uku. 1

“Fanya Yote Uwezayo Kabisa”

1 Tulipojitoa wakfu kwa Yehova, tulimuahidi kumtolea kutoka kwetu wenyewe kile kilicho bora iwezekanavyo. Ni kwa sababu hiyo, mtume Petro aliwatia Wakristo moyo kufanya yote wawezayo ili kukomaza uhusiano wao pamoja na Yehova. (2 Pt. 1:10) Tunataka hakika kufanya yote tuwezayo kabisa ili kumfurahisha Yehova kwa kumtumikia tangu sasa. Hilo linamaanisha nini? Kwa kadiri uhusiano wetu pamoja na Yehova unavyokuwa wa karibu zaidi na kwamba tunatafakari juu ya yote aliyofanya kwa ajili yetu, moyo wetu unatusukuma sikuzote kufanya tuwezayo katika utumishi wake. Tunataka kuboresha huduma yetu katika uzuri na, wakati inapowezekana, katika uwingi.—Zab. 34:8; 2 Tim. 2:15.

2 Ndugu mmoja kijana aliyetaka kutimiza mengi zaidi katika huduma aliona kwamba funzo la kawaida la Neno la Mungu lilikuwa likiongeza shukrani yake kwa Yehova na lilikuwa likimpa juhudi kubwa zaidi. Hilo lilimsukuma kujaza ombi kwa ajili ya utumishi wa painia. Dada mmoja aliyekuwa na magumu kuzungumza na watu asiojuana nao alitumikisha utoaji mbalimbali wa kitabu Kutoa Sababu, jambo ambalo lilimwezesha kupata haraka mafanikio mengi zaidi katika huduma. Aliweza kujifunza Biblia pamoja na wenzi wawili wa ndoa waliokubali ukweli.

3 Furahia Kile Unachoweza Kufanya: Wamoja kati yetu wanapatikana katika hali ngumu kwa sababu ya afya mbaya, upinzani wa familia, umaskini au ubaridi wa watu wa eneo. Matatizo mengine mengi, ya kawaida katika kipindi cha siku za mwisho, yanaweza kuzuia utumishi wetu. (Lk. 21:​34, nota; 2 Tim. 3:1). Je! hilo linamaanisha kwamba sisi si waaminifu kwa nadhiri tuliyofanya kwa Yehova? Sivyo, ikiwa tunafanya yote tuwezayo katika utumishi wake.

4 Haingekuwa hekima kujihukumu sisi wenyewe kwa kulinganisha na yale wengine wanayoweza kufanya. Badala yake, Maandiko yanamtia moyo kila mmoja wetu ‘athibitishe kazi yake mwenyewe ni nini’. Ikiwa tunajitoa kabisa kulingana na uwezo wetu mbalimbali wa kibinafsi, tutapata ukubali wa Yehova na tutapatia ndani shangwe.—Gal. 6:4; Kol. 3:23, 24.

5 Basi na tujali maneno ya Petro na ‘kufanya kabisa yote tuwezayo ili mwishowe tupatikane naye tukiwa bila doa na bila waa na katika amani.’ (2 Petro 3:​14, TUM) Hali hiyo itatuletea hisia moyoni yenye salama na amani ya roho ambayo Yehova peke yake ana uwezo wa kutoa.​—Zab. 4:8.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine