Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 5/98 uku. 1
  • Tuhudhurie Mikutano “Zaidi Sana”

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Tuhudhurie Mikutano “Zaidi Sana”
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Sababu Gani Tunapaswa Kukusanyika Pamoja Ili Kuabudu?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2016
  • Utapata Faida Gani Kama Unaenda ku Mikutano ya Mashahidi wa Yehova?
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
  • Mikutano hufaidi vijana
    Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Kuhuzuria Mikutano Kunaonyesha Nini Juu Yetu?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2019
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1998
km 5/98 uku. 1

Tuhudhurie Mikutano “Zaidi Sana”

1 Kukutanika pamoja kumekuwa sikuzote jambo la maana kwa watu wa Yehova. Waisraeli walikuwa na hekalu na masinagogi yao yakiwa vitovu vya ibada ya kweli, vya elimu ya kimungu, na ushirika wenye shangwe. Kwa sababu izohizo Wakristo wa mapema hawakuachilia mbali kukutanika pamoja. Kadiri mikazo na majaribu yanavyoongezeka katika siku hizi ngumu za mwisho, sisi pia tunahitaji utiwaji-nguvu wa kiroho ambao mikutano yetu ya kutaniko huandaa na tunahitaji huo “zaidi sana.” (Ebr. 10:25) Ona sababu tatu kwa nini tunahudhuria kwenye mikutano.

2 Kwa Ajili ya Ushirika: Maandiko yanatusihi “[tu]fulize kufarijiana na kujengana.” (1 Thes. 5:​11) Ushirika wa kimungu unajaza akili zetu kwa mawazo mazuri na hutusukuma kufanya kazi njema. Lakini ikiwa tunajitenga wenyewe, tunakuwa wepesi kufikiria mawazo ya kipumbavu, ya uchoyo, na hata yasiyo ya adili.​—Mez. 18:1.

3 Kwa Ajili ya Maagizo: Mikutano ya Kikristo huandaa programu yenye kuendelea ya maagizo ya kibiblia yanayokusudia kudumisha upendo kwa Yehova ukiwa hai katika mioyo yetu. Inatoa mwongozo wenye kutenda katika kutumia “shauri lote la Mungu.” (Mdo. 20:27) Mikutano hutuzoeza ufundi wa kuhubiri na kufundisha habari njema, ustadi unaohitajiwa zaidi sana leo ili kuhisi furaha isiyoweza kusimuliwa ya kupata na kusaidia wale watakaokubali ukweli wa Biblia.

4 Kwa Ajili ya Ulinzi: Katika ulimwengu huu mwovu, kutaniko ni kimbilio la kweli la kiroho​—kituo chenye amani na upendo. Wakati tunaposhiriki mikutano, roho takatifu ya Mungu huwa na uvutano wenye nguvu juu yetu, ikitokeza matunda ya “upendo, shangwe, amani, ustahimilivu, fadhili, wema, imani, upole, kujidhibiti.” (Gal. 5:​22, 23) Mikutano hututia nguvu kusimama imara na wenye nguvu katika imani. Inatuandalia vifaa ili kututayarisha kwa ajili ya majaribu yaliyo mbele.

5 Kwa kuhudhuria mikutano kikawaida, tunahisi yale mtunga-zaburi aliyoeleza, kama yanavyorekodiwa kwenye Zaburi 133:​1, 3: “Tazama, ni wema na ya kupendeza sana kwa ndugu kukaa pamoja kwa umoja!” Mahali popote watu wa Mungu wanapotumikia na kukutana pamoja leo, “pale BWANA [Yehova, NW] aliamuru baraka, hata uzima kwa milele.”

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine