Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 9/00 uku. 8
  • “Je, ninapaswa kuhama?”

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • “Je, ninapaswa kuhama?”
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Uhamie Kwenye Kuwa Lazima Kubwa ya Wahubiri
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2022
  • Je, Unaweza ‘Kuvuka Uingie Makedonia’?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Namna ya Kupanua Utumishi Wako
    Tengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova
  • Mlango Mkubwa Kuelekea Utendaji Umefunguliwa
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2000
km 9/00 uku. 8

“Je, ninapaswa kuhama?”

1 Katika kuitikia amri ya Yesu ya ‘kwenda . . . kufanya wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote,’ watumishi wengi wa Yehova walio wakfu wamehama ili kutumikia mahali ambako uhitaji ni mkubwa zaidi. (Mt. 28:19) Wanaiga Paulo, aliyeitikia mwito: “Vuka uingie Makedonia utusaidie.” (Mdo. 16:9) Hilo linaweza kufanywaje kwa njia yenye kufaa?

2 Timiza hatua moja moja: Je, kuna eneo lisilotumikwa kikawaida katika kutaniko lenu? Ikiwa ni hivyo, unaweza kukaza jitihada zako juu ya maeneo hayo. Kabla ya kuamua kwenda mahali pengine, zungumza na wazee wenu ili uone ikiwa wanafikiri kwamba una vifaa kwa ajili ya kuhama. Unaweza pia kuuliza mwangalizi wa mzunguko wenu ikiwa anajua kutaniko la kando-kando ambako unaweza kupanua huduma yako. Kwa upande mwingine, baada ya kuhesabu gharama kwa uangalifu, unaweza kutaka kufikiria kusaidia katika sehemu nyingine ya nchi au katika nchi nyingine. Ikiwa hiyo ndiyo tamaa yako, wewe pamoja na baraza lenu la wazee mnapaswa kuandikia ofisi ya tawi ambako unapenda kutumikia, mkionyesha hali yako ya kitheokrasi. Linaweza kuwa jambo la hekima kutembelea eneo lenyewe kabla ya kuamua kuhama au kutohama kwa wakati wote.

3 Iweni waangalifu kuhusu kuhamia nchi nyingine: Hesabu yenye kuongezeka ya ndugu zetu ni wenye kuhamia nchi nyinginezo kwa sababu wanatafuta maisha mazuri zaidi au kitulizo kutokana na uonevu. Wanapokuwa wakihama, wengine wameangukia mikononi mwa watu wasio na haya ambao wanaahidi kuwasaidia wakae katika ile nchi mpya lakini ambao huchukua tu fedha zao na kisha huwaacha. Katika hali fulani watu hao hujaribu hata kukaza wahamiaji ili kuwaingiza katika utumwa wa mambo yasiyo ya adili. Wakati wanapokataa, wao huwaacha wakiwatupia nchi ambayo wameingia. Hivyo, hali ya wahamiaji hao imekuwa mbaya zaidi kuliko ilivyokuwa katika nchi yao. Wanaweza hata kuhitaji kuomba akina ndugu wawape mahali pa kukaa na kuwasaidia kwa njia nyingine, wakitia mzigo juu ya familia nyinginezo za Kikristo ambazo zinapigana na matatizo na magumu yazo zenyewe. Washiriki wa familia fulani wametenganishwa kimwili, na familia zimedhoofishwa kiroho kwa sababu ya uhamiaji huo usio wa hekima.—1 Tim. 6:8-11.

4 Ikiwa mnataka kuhama kwa ajili ya faida ya kibinafsi, lindeni akilini kwamba mahali popote mnapoishi, kuna matatizo ya kukabiliana nayo. Ni rahisi zaidi kushinda matatizo mahali ambapo tayari mnajua lugha na desturi za watu, badala ya kuanza upya katika mazingira msiyoyajua.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine