Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 3/01 uku. 8
  • Saidieni wengine wahudhurie mikutano

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Saidieni wengine wahudhurie mikutano
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2001
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Tuwaongoze Wanafunzi Kwenye Tengenezo La Yehova
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Saidia Mwanafunzi Wako wa Biblia Afikie Kubatizwa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2021
  • Utapata Faida Gani Kama Unaenda ku Mikutano ya Mashahidi wa Yehova?
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
  • Namna ya Kusaidia Wanafunzi wa Biblia Wafikie Kubatizwa—Sehemu ya Kwanza
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2001
km 3/01 uku. 8

Saidieni wengine wahudhurie mikutano

1 “Marafiki wowote katika ujirani . . . wanaotaka kuhudhuria mikutano wanaalikwa kwa shauku wafanye hivyo.” Sikuzote tangu tangazo hilo lilipotokea katika toleo la Novemba 1880 la Phare de la Tour de Sion, Mashahidi wa Yehova wamealika kwa shauku watu wakusanyike pamoja kwa ajili ya maagizo ya Biblia. (Ufu. 22:17) Hiyo ni sehemu ya maana ya ibada ya kweli.

2 Ni jambo la maana sana kuhudhuria: Tunapata baraka wakati tunaposhirikiana na kutaniko. Tunapata kujua vizuri zaidi Mungu wetu wa ajabu, Yehova. Katika kutaniko, tunakutana pamoja ili ‘kufundishwa na Yehova.’ (Isa. 54:13) Tengenezo lake linatoa kwa kifupi programu yenye kuendelea ya mafundisho ya Biblia, programu inayotuvuta karibu zaidi naye na inayotoa msaada wenye kutumika kuhusu jinsi ya kutumikisha “shauri lote la Mungu.” (Mdo. 20:27; Luka 12:42) Mikutano hutoa mazoezi ya kibinafsi katika ufundi wa kufundisha Neno la Mungu. Vikumbusho kutoka katika Maandiko vinatusaidia kufurahia uhusiano wenye mafanikio pamoja na wengine na pamoja na Yehova mwenyewe. Kushirikiana na wale wanaopenda Yehova hutia nguvu imani yetu.—Rom. 1:11, 12.

3 Toeni mwaliko wa moja kwa moja: Kuanzia funzo la kwanza, alika kila mwanafunzi wa Biblia kwenye mikutano. Amsha kupendezwa kwake kwa kushiriki jambo moja lililokutia moyo kutokana na mkutano wa mwisho na kwa kufikiria jambo fulani litakalozungumziwa kwenye mkutano unaokuja. Eleza jinsi Jumba la Ufalme lilivyo, na uhakikishe kwamba anajua jinsi ya kulipata.

4 Ikiwa mwanafunzi hahudhurii papo hapo, endelea kumwalika. Chukua dakika chache kila juma ili kumwonyesha jinsi tengenezo letu linavyofanya kazi. Tumia broshua Wanafanya Mapenzi ya Mungu na vidio Les Témoins de Jéhovah : un nom, une organisation ili kufanya atujue na kujua mikutano yetu. Peleka wahubiri wengine pamoja nawe ili kufanya mwanafunzi apate kujuana nao. Katika sala, mshukuru Yehova kwa tengenezo na useme kuhusu uhitaji wa mwanafunzi kushirikiana nalo.

5 Msisite kusaidia wale waliopendezwa karibuni wakusanyike pamoja nasi. Kadiri uthamini wao kuelekea Yehova unavyokomaa, watachochewa kutumikisha yale wanayojifunza na kuwa sehemu ya tengenezo la Mungu lenye umoja.—1 Kor. 14:25.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine