Kila Mmoja Anaweza Kujifunza Kutokana na Vidio Noé : il marchait avec Dieu
Soma au rudilia Mwanzo 6:1 mpaka 9:19. Kisha tazama vidio Noé, na ufikirie jinsi unavyoweza kujibu maulizo haya: (1) Ulimwengu ulikuwa namna gani katika siku ya Noa, nao ulifikiaje hali hiyo? (2) Ni nini kilichomfanya Noa awe mtu wa pekee sana, ni kazi gani ambayo Mungu alimpa afanye, na kwa nini? (3) Yaelekea safina ilijengwa wapi, ilichukua muda gani, nayo ilikuwa na ukubwa kiasi gani? (4) Zaidi ya kujenga safina, ni nini lingine ambalo Noa na familia yake walipaswa kufanya? (5) Unafikiri hali ilikuwa namna gani ndani ya safina wakati mlango ulipofungwa? (6) Ungejisikia namna gani baada ya kuokoka ile Gharika? (7) Ni kikumbusho gani cha Gharika tunachokiona pindi kwa pindi, nacho kinamaanisha nini? (8) Simulizi la Biblia kuhusu Noa limekufundisha nini kuhusu wewe mwenyewe, familia yako, na kazi ambayo Mungu ametutolea tufanye? (9) Ni maulizo gani utakayotaka kuuliza Noa na familia yake utakapokutana nao katika Paradiso? (10) Unapanga kutumiaje sasa vidio Noé?