Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 9/02 uku. 1
  • Tusaidie Wengine Wamtukuze Yehova

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Tusaidie Wengine Wamtukuze Yehova
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Sababu Gani Tunapaswa Kulitumia Jina la Mungu?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Jina la Mungu
    Amuka!—2017
  • Tuliheshimu Jina Kubwa la Mungu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • “Unganisha Moyo Wangu ili Niogope Jina Lako”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2002
km 9/02 uku. 1

Tusaidie Wengine Wamtukuze Yehova

1 Ujumbe wa maana sana unatangazwa kwa watu duniani pote: “Hofuni Mungu na kumpa utukufu, kwa sababu saa ya hukumu yake imewasili, na kwa hiyo mwabuduni Yeye aliyezifanya mbingu na dunia na bahari na mabubujiko ya maji.” (Ufu. 14:6, 7) Ni pendeleo letu kushiriki tangazo hilo. Watu wanahitaji kujua nini kuhusu Yehova ili wamwogope na kumwabudu?

2 Jina Lake: Watu wanahitaji kuweza kutofautisha kwa jina Mungu wa pekee wa kweli na ile miungu mingi ya uwongo inayoabudiwa leo. (Kum. 4:35; 1 Kor. 8:5, 6) Kwa kweli, waandikaji wa Biblia walitumia jina tukufu la Yehova mara zaidi ya 7,000. Ingawa tunatumia utambuzi ili kuamua wakati wa kujulisha watu jina la Mungu, hatupaswi kamwe kulificha au kujizuiza kulitumia. Mapenzi ya Mungu ni kwamba wanadamu wote wapate kujua jina lake.—Zab. 83:18.

3 Utu Wake: Ili kumtukuza Yehova, watu wanahitaji kujua yeye ni Mungu wa aina gani. Tunapaswa kuwasaidia wajue upendo wake wenye kutokeza, hekima yake iliyo bora zaidi, haki yake kamili, na nguvu zake zenye uweza wote, pamoja na rehema yake, fadhili zake zenye upendo, na sifa zake nyingine bora. (Kut. 34:6, 7) Wanapaswa pia kujifunza kuwa na woga wa Mungu unaofaa, na kumheshimu sana, wakitambua ya kwamba maisha yao yenyewe yanategemea kuwa na ukubali wa Yehova.—Zab. 89:7.

4 Kumkaribia Sana Mungu: Ili kuokoka hukumu ya Mungu inayokuja, watu wanapaswa kuitia Yehova kwa imani. (Rom. 10:13, 14; 2 Thes. 1:8) Hilo linatia ndani mengi zaidi ya kupata kujua tu jina la Mungu na sifa zake. Tunapaswa kusaidia watu wasitawishe uhusiano wa kibinafsi pamoja na Yehova, wakimtumainia kwa moyo wao wote. (Mez. 3:5, 6) Wanapotumia yale wanayojifunza, wanapomwendea Mungu katika sala yenye bidii, na wanapoona jinsi anavyowasaidia maishani mwao, imani yao itakomaa, ikiwasaidia wamkaribie Yehova.—Zab. 34:8.

5 Acheni tutangaze kwa bidii jina la Mungu na kusaidia wengine wamtumaini kikamili na kumwogopa. Huenda tukaweza kusaidia watu wengi zaidi wapate kumjua Yehova na kumtukuza kuwa “Mungu wa wokovu” wao.—Zab. 25:5.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine