Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 12/02 uku. 1
  • Kumbukeni Wazee-Wazee Walio Waaminifu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kumbukeni Wazee-Wazee Walio Waaminifu
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Uone Ndugu na Dada Wenye Walishazeeka Kuwa wa Maana Sana
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2021
  • Mutumikie Yehova Mbele ya Siku Zenye Musiba
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Unaweza Kumualika Muhubiri Mwengine?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2013
  • Tuwaheshimu Ndugu na Dada Zetu Wenye Kuzeeka
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
Huduma Yetu ya Ufalme—2002
km 12/02 uku. 1

Kumbukeni Wazee-Wazee Walio Waaminifu

1 Ingawa alikuwa mjane na mwenye kuzeeka, Ana mwenye umri wa miaka 84 “alikuwa hakosi kamwe kuwa katika hekalu.” Uaminifu wake ulimsukuma Yehova ampe thawabu ya pekee. (Luka 2:36-38) Leo, ndugu na dada wengi wanaonyesha roho kama ile ya Ana ijapokuwa wanapambana na hali ngumu. Waaminifu hao wanapolazimika kupambana na matatizo ya afya au vizuizi vinavyotokana na uzee, wanaweza nyakati nyingine kujisikia wenye kuvunjika moyo. Acheni tuchunguze njia fulani zenye kutumika ambazo katika hizo tunaweza kuwatia moyo na kuwasaidia walinde kawaida nzuri ya kiroho.

2 Mikutano na Huduma: Wengine wanapopendekeza kwa upendo kutoa chombo cha kusafiria, wazee-wazee wengi walio waaminifu wanaweza kwa vyepesi zaidi kuhudhuria mikutano ya Kikristo kwa ukawaida. Hilo linajenga hali ya kiroho ya watumishi hao waaminifu na wa muda mrefu na linafaidi kutaniko vilevile. Je, umekwisha kushiriki kazi hiyo njema?—Ebr. 13:16.

3 Kushiriki kikawaida katika huduma kunaletea Wakristo furaha ya kweli na kutosheka. Lakini kufanya hivyo kunaweza kuwa jambo gumu kwa wazee-wazee na kwa wale wasiojiweza. Je, inawezekana mmoja wa wapendwa hao aandamane nawe katika sehemu fulani ya kazi ya kutoa ushahidi akiwa ‘mfanyakazi mwenzako’? (Rom. 16:3, 9, 21) Labda unaweza kumwalika ashiriki nawe kutoa ushahidi kwa njia ya simu au kwenda nawe kwenye ziara ya kurudia au funzo la Biblia. Ikiwa yule aliye mzee-mzee hawezi kutoka nyumbani, je, mwanafunzi wa Biblia anaweza kuja nyumbani kwa mtu huyo kwa ajili ya mafunzo?

4 Funzo na Ushirika: Mara kwa mara, watu fulani hualika ndugu au dada mzee-mzee au asiyejiweza ashiriki funzo lao la familia, na hata kufanyia funzo hilo nyumbani mwake. Mama mmoja alipeleka watoto wake wawili wachanga nyumbani kwa dada mzee-mzee kwa ajili ya funzo lao katika Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia, na wote walitiwa moyo na ushirika. Watu kama hao hufurahia pia kualikwa kwa ajili ya chakula au tukio lingine pamoja na marafiki. Ikiwa watu wasiojiweza ni dhaifu sana hivi kwamba hawawezi kufanyiwa ziara ndefu, labda unaweza kuwatembelea kwa muda mfupi ili kuwasomea, kusali pamoja nao, au kushiriki nao jambo lililoonwa lenye kujenga—Rom. 1:11, 12.

5 Yehova anathamini sana wazee-wazee walio waaminifu. (Ebr. 6:10, 11) Tunaweza kumwiga kwa kuonyesha uthamini wetu kwao na kwa kuwasaidia walinde kawaida nzuri ya kiroho.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine