Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 4/03 uku. 1
  • ‘Lifanyie Hilo Nafasi’

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • ‘Lifanyie Hilo Nafasi’
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Tumia Vizuri Kabisa Useja Wako
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Maulizo ya Wasomaji Wetu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Mashauri ya Hekima Kuhusu Useja na Ndoa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Faida ya Kubakia Bila Kuoa ao Kuolewa
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2019
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2003
km 4/03 uku. 1

‘Lifanyie Hilo Nafasi’

1 Wakati fulani, alipokuwa akisema na wanafunzi wake kuhusu ndoa, Yesu alitaja useja kuwa “zawadi.” Kisha akasema: “Acheni yeye awezaye kufanyia hilo nafasi alifanyie hilo nafasi.” (Mt. 19:10-12) Miaka fulani baadaye, mtume Paulo aliandika kuhusu faida zinazotokana na useja na akatia wengine moyo wafuate mfano wake kwa kubaki wasiofunga ndoa. (1 Kor. 7:7, 38) Wengi leo ‘wamefanyia useja nafasi’ na wanafurahia faida zinazotokana na huo. Ni nini faida fulani kati ya hizo?

2 Kutumika “Bila Kukengeushwa Fikira”: Paulo alielewa kwamba useja ulimpa nafasi ya kutumikia Yehova “bila kukengeushwa fikira.” Vivyo hivyo leo, ndugu aliye mseja anaweza kufanya jitihada za kuhudhuria Shule ya Mazoezi ya Kihuduma, na mseja kwa kawaida yuko huru zaidi kuanza kazi ya painia, kujifunza lugha nyingine, kuhamia mahali ambapo uhitaji ni mkubwa zaidi, kutumikia Betheli, au kuwa tayari kwa ajili ya mapendeleo mengine ya pekee ya utumishi. Anaweza kuwa na wakati na nafasi zaidi ya kufanya funzo la kibinafsi na kutafakari kwa kina kirefu na kuzungumza na Yehova katika sala ya kutoka moyoni. Kwa kawaida mtu asiyefunga ndoa ana wakati zaidi wa kujitoa ili kusaidia wengine. Utendaji wote huo ni kwa ‘faida yake ya kibinafsi.’—1 Kor. 7:32-35; Mdo. 20:35.

3 Utumishi huo kwa Mungu usiokengeuka unaleta thawabu zenye kutajirisha. Baada ya miaka 27 huko Kenya, dada mmoja mseja aliandika: “Kulikuwa na marafiki wengi na kazi nyingi! Tulifanya mambo pamoja [na] kutembeleana. . . . Niliweza kutumia ule uhuru na urahisi wa kusafiri unaotolewa na useja ili kuendelea kuwa na shughuli nyingi katika huduma, na hilo limenipa furaha nyingi sana.” Akaongeza: “Kwa muda wa miaka iliyopita uhusiano wangu pamoja na Yehova umeimarika.”

4 Kulifanyia Nafasi: Yesu alisema kwamba kichocheo cha kusitawisha zawadi ya useja kingepaswa kuwa “kwa sababu ya ufalme wa mbingu.” (Mt. 19:12) Kama ilivyo kuhusu zawadi yoyote, useja unapaswa kutumiwa inavyofaa ili kuleta shangwe na faida. Kwa kutumia vizuri nafasi zinazotokezwa na useja na kwa kumtegemea Yehova ili kupata hekima na nguvu, watu wengi wasiofunga ndoa wamekuja kuelewa thamani ya kufanyia zawadi hiyo nafasi.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine