Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 9/03 uku. 1
  • Jivikeni Unyenyekevu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Jivikeni Unyenyekevu
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Yehova Anaona Watumishi Wake Wanyenyekevu Kuwa wa Maana
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2019
  • Yesu Alituachia Mufano Wa Unyenyekevu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Usijifikirie Mwenyewe Sana Kuliko Vile Inaomba Kufikiri
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
  • Tuonyeshe Sifa Zenye Kumupendeza Mungu—Unyenyekevu
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2017
Huduma Yetu ya Ufalme—2003
km 9/03 uku. 1

Jivikeni Unyenyekevu

1 Mvulana mchungaji amtumaini Yehova na kumshinda mpiganaji mwenye nguvu. (1 Sam. 17:45-47) Mwanamume mwenye mali nyingi avumilia msiba. (Yobu 1:20-22; 2:9, 10) Mwana wa Mungu ampelekea Baba yake sifa zote zinazotokana na ufundishaji wake. (Yoh. 7:15-18; 8:28) Katika kila mmoja wa mifano hiyo, unyenyekevu ulitimiza fungu la maana sana. Vivyohivyo leo, unyenyekevu ni wa maana sana katika hali tunazopambana nazo.—Kol. 3:12.

2 Tunapohubiri: Tukiwa wahudumu Wakristo, tunashiriki kwa unyenyekevu habari njema na watu wa aina zote, bila kuwahukumu kimbele kwa msingi wa rangi, wa utamaduni, au wa malezi. (1 Kor. 9:22, 23) Ikiwa watu fulani ni wenye kukosa adabu au wanakataa kwa kiburi ujumbe wa Ufalme, hatuitikii kwa njia hiyohiyo lakini kwa uvumilivu tunaendelea kutafuta wale wanaostahili. (Mt. 10:11, 14) Badala ya kujaribu kufanya wengine waone ujuzi wetu au elimu yetu, tunaelekeza uangalifu kwa Neno la Mungu, tukijua kwamba ni lenye kusadikisha zaidi kuliko jambo lolote tunaloweza kusema. (1 Kor. 2:1-5; Ebr. 4:12) Kwa kuiga Yesu, tunampa Yehova sifa yote.—Marko 10:17, 18.

3 Katika Kutaniko: Wakristo wanapaswa pia ‘kujifunga hali ya akili ya kujishusha chini kuelekea mtu na mwenzake.’ (1 Pet. 5:5) Ikiwa tunawaona wengine kuwa wa hali ya juu kuliko sisi, tutatafuta njia za kutumikia ndugu zetu badala ya kuwatazamia wao watutumikie. (Yoh. 13:12-17; Flp. 2:3, 4) Hatutafikiri kwamba hatustahili kufanya kazi kama vile kusafisha Jumba la Ufalme.

4 Unyenyekevu unatusaidia ‘tuchukuliane mtu na mwenzake katika upendo’ na hivyo unaendeleza amani na umoja katika kutaniko. (Efe. 4:1-3) Unatusaidia tujitiishe kwa wale waliowekwa rasmi ili kuongoza. (Ebr. 13:17) Unatuchochea tukubali shauri au nidhamu yoyote tunayoweza kupewa. (Zab. 141:5) Na unyenyekevu unatuchochea tutegemee Yehova tunaposhughulikia mapendeleo yoyote tunayoweza kupokea katika kutaniko. (1 Pet. 4:11) Kama Daudi, tunatambua kwamba kufanikiwa hakutegemei uwezo wa kibinadamu lakini kunategemea baraka za Mungu.—1 Sam. 17:37.

5 Mbele za Mungu Wetu: Zaidi ya yote, tunahitaji ‘kujinyenyekeza chini ya mkono wa Mungu wenye uweza.’ (1 Pet. 5:6) Ikiwa tunapambana na hali zenye kujaribu, tunaweza kutamani sana kitulizo ambacho Ufalme utaleta. Lakini kwa unyenyekevu tunajizoeza uvumilivu, tukingojea Yehova atimize ahadi zake kwa wakati wake. (Yak. 5:7-11) Kama ilivyokuwa kweli kuhusu Yobu aliyeshika uaminifu wa maadili, hangaiko letu kubwa zaidi ni kwamba ‘jina la Yehova libarikiwe.’—Yobu 1:21.

6 Nabii Danieli ‘alijinyenyekeza mbele ya Mungu wake’ na alikubaliwa na Yehova na kupewa mapendeleo mengi bora. (Dan. 10:11, 12) Acheni sisi pia tujivike unyenyekevu, tukijua kwamba “zawabu ya unyenyekevu na woga wa BWANA ni mali na heshima na uzima.”—Mit. 22:4.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine