Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 7/04 uku. 1
  • Tuige Haki ya Yehova

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Tuige Haki ya Yehova
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2004
Huduma Yetu ya Ufalme—2004
km 7/04 uku. 1

Tuige Haki ya Yehova

1 “Yehova ni mpenda-haki.” (Zab. 37:28) Hivyo, ingawa ameamua kwamba ulimwengu huu usio na uadilifu uangamizwe, amefanya mpango ili onyo litolewe kwanza. (Marko 13:10) Jambo hilo linatolea watu nafasi ya kutubu na kuokolewa. (2 Pet. 3:9) Je, tunajitahidi kuiga haki ya Yehova? Je, taabu na mateso ya familia ya kibinadamu vinatuchochea kushiriki tumaini la Ufalme na wengine? (Met. 3:27) Kupenda haki kutatuchochea kushiriki kwa bidii kazi ya kuhubiri.

2 Tuhubiri Bila Upendeleo: Tunapotangaza kusudi la Mungu kwa kila mtu bila upendeleo, ‘tunatenda haki.’ (Mika 6:8) Tunapaswa kupinga mwelekeo usio mkamilifu wa kuhukumu kimbele wengine kulingana na hali yao ya nje. (Yak. 2:1-4, 9) ‘Mapenzi ya Yehova ni kwamba watu wa namna zote waokolewe na kupata ujuzi sahihi wa kweli.’ (1 Tim. 2:4) Neno la Mungu la kweli linaweza kuongoza watu kufanya mabadiliko makubwa maishani mwao. (Ebr. 4:12) Kuelewa jambo hilo kutatuchochea tuendee watu, hata wale ambao huenda wamekataa kusikiliza wakati uliopita, tukiwa na uhakika.

3 Dada mmoja mwenye kutumika dukani aliogopeshwa kwa kadiri fulani na sura au maumbile ya mnunuzi fulani aliyekuwa akiwanunulia vitu kwa kawaida. Hata hivyo, nafasi inayofaa ilipojitokeza, dada alijaribu kumtolea ushahidi kuhusu Paradiso iliyoahidiwa na Mungu. Akamjibu kwa kumkatiza kwamba yeye haamini hadithi zinazotungwa ili kudanganya watu na kwamba yeye ni hipi na mzoevu wa dawa za kulevya. Lakini dada huyo hakukata tamaa. Siku moja mnunuzi huyo akamuuliza maoni yake kuhusu nywele zake ndefu, naye dada akaeleza kwa busara yale ambayo Biblia inasema kuhusu jambo hilo. (1 Kor. 11:14) Siku ifuatayo, dada huyo alifurahi kwa mshangao alipomwona akiwa na ndevu zimenyolewa vizuri na mwenye nywele fupi! Akaomba funzo la Biblia, ambalo ndugu mmoja alifurahia kuongoza, naye mtu huyo akafanya maendeleo kufikia wakfu na ubatizo. Kama mwanamume huyo, wengi wanaomtumikia Yehova leo ni wenye shukrani kuhusu jitihada zisizo na upendeleo na zenye kudumu za wale waliowaletea ujumbe wa Ufalme.

4 Hivi karibuni, Yehova atakomesha ukosefu wa uadilifu duniani pote. (2 Pet. 3:10, 13) Katika wakati mfupi unaobaki, na tuige haki ya Yehova tukitolea wote nafasi ya kuepuka uharibifu unaokuja wa ulimwengu wa Shetani usio na uadilifu.—1 Yoh. 2:17.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine