Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 12/04 uku. 8
  • Kutolea Watu wa Jamaa Ushahidi—Jinsi Gani?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kutolea Watu wa Jamaa Ushahidi—Jinsi Gani?
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Jinsi Gani Kutendea Familia Yetu?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Namna ya Kugusa Mioyo ya Watu wa Jamaa Wasio Mashahidi
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • “Wale Wenye Wanakusikiliza” Wataokolewa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2019
  • Kweli Hailete, “Amani, Bali Upanga”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2017
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2004
km 12/04 uku. 8

Kutolea Watu wa Jamaa Ushahidi—Jinsi Gani?

1 Jinsi ingekuwa furaha kubwa kabisa kuingia katika ulimwengu mpya pamoja na wapendwa wetu, tukiungana nao katika ibada ya Yehova! Tukitolea watu wa jamaa yetu ushahidi, tumaini hili lenye kufurahisha linaweza kuwa jambo halisi. Hata hivyo, kutolea watu wa jamaa ushahidi kwa namna yenye kuburudisha, kunaomba utambuzi. Mwangalizi mmoja wa mzunguko alieleza: “Wale ambao pindi kwa pindi wanazungumzia vichwa vinavyoamsha kupendezwa kwa watu wa jamaa, wanapata matokeo bora zaidi.” Tunaweza namna gani kufanya hivyo?

2 Amsha Kupendezwa Kwao: Fikiria kwa makini jinsi unavyoweza kuamsha kupendezwa kwa watu wa jamaa. (Met. 15:28) Ni nini mahangaiko yao? Ni magumu gani wanayopambana nayo? Labda unaweza kuwaonyesha makala moja au kutaja andiko moja lenye kuvutia kuhusu habari inayowapendeza kibinafsi. Ikiwa watu wa jamaa yako hawaishi karibu, labda unaweza kufanya hivyo kwa njia ya barua au ya simu. Bila kuwasumbua, panda mbegu ya kweli, na umtegemee Yehova ili akuze mbegu hizo.—1 Kor. 3:6.

3 Yesu aliagiza mtu mmoja ambaye kutoka kwake alifukuza roho waovu wengi: “Nenda nyumbani kwa watu wa jamaa yako, ukawaambie mambo yote ambayo Yehova amekufanyia na jinsi alivyokuonyesha rehema.” (Marko 5:19) Wazia jinsi watu wa jamaa yake walivyojisikia! Ijapokuwa huenda usikutane na jambo lolote lenye kutokeza kama hilo, yaelekea kwamba watu wa jamaa yako wanapendezwa na utendaji wako au ule wa watoto wako. Kusemea hotuba uliyotoa kwenye Shule ya Huduma ya Kitheokrasi, mkusanyiko uliohudhuria, ziara uliofanya kwenye Betheli, au tukio moja lenye maana kunaweza kukufungulia njia ya kuzungumza nao jambo fulani zaidi kumhusu Yehova na tengenezo lake.

4 Uwe Mwenye Utambuzi: Unapotoa ushahidi kwa watu wa jamaa, epuka kuwaambia mambo mengi mno mara moja. Akikumbuka wakati alipoanza kujifunza Biblia, ndugu mmoja alisema: “Ndipo kwa muda wa saa nyingi nikamumiminia mama yangu maelezo kuhusu karibu kila jambo nililojifunza kutoka katika Biblia, na mara nyingi hilo liliongoza kwenye mabishano, hasa na baba yangu.” Hata mtu wa jamaa anapoonyesha kupendezwa na ujumbe wa Biblia, mjibu kwa namna itakayomfanya apende kujua mengi zaidi. (Met. 25:7) Sikuzote onyesha heshima, fadhili, na uvumilivu, kama vile unavyofanya unapozungumza na wageni katika huduma.—Kol. 4:6.

5 Kwenye pindi moja, watu wa jamaa ya Yesu walifikiri kwamba alipoteza akili. (Marko 3:21) Hata hivyo, baadaye, wamoja walifikia kuwa waamini. (Mdo. 1:14) Ikiwa jitihada zako za mwanzo za kushiriki kweli pamoja na watu wa jamaa yako hazifanikiwi, usiache. Hali na mitazamo yao inaweza kubadilika. Endelea kutafuta nafasi nyingine ili kuwaelezea kuhusu jambo fulani linaloweza kuamsha kupendezwa kwao. Unaweza kupata furaha inayotokana na kuwasaidia waanze kutembea katika barabara inayoongoza kwenye uzima wa milele. —Mt. 7:13, 14.

[Maulizo ya Funzo]

1. Kwa nini utambuzi unahitajiwa tunapotolea watu wa jamaa ushahidi?

2. Jinsi gani kupendezwa kikweli na watu wa jamaa zetu kunavyoweza kutusaidia tuamshe kupendezwa kwao?

3. Jinsi gani kule kupendezwa nasi kwa watu wa jamaa yetu kunavyoweza kutufungulia njia ya kutoa ushahidi?

4. Ni mitego gani tunayopaswa kuepuka tunapotolea watu wa jamaa ushahidi?

5. Tutafanya nini ikiwa watu wa jamaa yetu hawaitikii inavyofaa tunapowatolea ushahidi?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine