Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 3/05 uku. 5
  • Vidio Iliyo na Ujumbe Wenye Kudumu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Vidio Iliyo na Ujumbe Wenye Kudumu
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2005
  • Habari za Kufanana na Zile
  • “Unifundishe Kufanya Mapenzi Yako”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • “Vita Ni vya Yehova”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2016
  • Daudi na Sauli
    Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
Huduma Yetu ya Ufalme—2005
km 3/05 uku. 5

Vidio Iliyo na Ujumbe Wenye Kudumu

Ni ujumbe gani ulio katika vidio David : il mettait sa confiance en Dieu ? (Daudi: Alimtegemea Mungu?) Kama Daudi, tunapaswa kumtegemea Yehova. (Zab. 91:2) Kwa kutazama matukio ya maana ya maisha ya Daudi yanayozungumziwa katika vidio hiyo, kutasaidia watoto na watu wazima kujifunza kutokana na mfano alioutoa. (Zab. 31:14) Ili itufaidi zaidi, DVD hii inatia ndani “Maulizo” na “Mambo Mbalimbali Yenye Kufundisha.”

Tazama vidio, na kisha ujiulize: (1) Kwa nini Yehova alichagua mfalme bora? (1 Sam. 15:10, 11; 16:1) (2) Kwa nini hakuchagua yeyote kati ya ndugu za Daudi? (1 Sam. 16:6, 7) (3) Kwa nini Saulo alipenda Daudi apige kinubi? (1 Sam. 16:14-23) (4) Goliathi alikuwa nani? (1 Sam. 17:4-10) (5) Kwa nini Daudi alipenda kumpiganisha Goliathi? (1 Sam. 17:23, 24, 36, 37) (6) Yonathani alikuwa nani? (1 Sam. 14:1) (7) Ni kwa kiasi gani Saulo alikuja kuwa adui mkubwa zaidi wa Daudi? (1 Sam. 18:25-29) (8) Kwa nini Daudi hakumuua Saulo? (1 Sam. 26:7-11)

(9) Saulo alikufa namna gani? (1 Sam. 31:1-6)

(10) Itikio la Daudi lilikuwa nini kuhusu kifo cha Yonathani? (2 Sam. 1:11, 12)

(11) Ni ahadi gani ambayo Yehova alimtolea Daudi? (2 Sam. 7:12, 13, 16) (12) Ni kosa gani nzito ambalo Daudi alifanya? (2 Sam. 11:1-5, 14-17) (13) Daudi alionyeshaje kwamba alihuzunika sana kwa sababu ya jambo alilofanya? (Zab. 51) (14) Ni somo gani mbalimbali ambazo Daudi alimfundisha kijana Solomono? (1 Fal. 2:1-4; 1 Nya. 22:6-13; 28:9, 10) (15) Namna gani utawala wa Yesu utafaidi Daudi, Yonathani, na wewe?—Isa. 11:6-9; Yoh. 11:25, 26.

Sasa fikiri kwa uzito: Daudi alimtegemea Mungu; unawezaje kibinafsi kuiga jambo hilo?

Wazazi, mkazie katika watoto wenu umaana wenye kudumu wa kumtumaini Mungu, kama Daudi alivyofanya.—Zab. 56:11.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine