Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 11/06 uku. 1
  • Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2006
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Kitabu ya Ufunuo​—Iko na Maana Gani Kwako Leo?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2022
  • Kitabu ya Ufunuo—Iko na Maana Gani Juu ya Wakati Wako Wenye Kuya?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2022
  • Tutoe Habari Njema, Tukitambua Kwamba Wakati Unasonga Mbele
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
Huduma Yetu ya Ufalme—2006
km 11/06 uku. 1

Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!

1 “Mwenye furaha ni yeye anayesoma kwa sauti na wale wanaosikia maneno ya unabii huu, na wanaoshika mambo yaliyoandikwa humo; kwa maana wakati uliowekwa uko karibu.” (Ufu. 1:3) Maneno hayo yanaonyesha kwamba kitabu cha Ufunuo ni cha maana sana, hasa kwa kuwa tunaishi katika wakati uliowekwa ili unabii mbalimbali wa kitabu hicho utimiye. Kwa kufaa, tutaanza kujifunza kitabu Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu! kwenye Funzo la Kitabu la Kutaniko katika juma linaloanza tarehe 8 mwezi wa 1, 2007.

2 Tangu tulipojifunza kitabu Ufunuo kwa mara ya mwisho kwenye Funzo la Kitabu la Kutaniko, mambo ya ulimwengu yamebadilika kwa namna nyingi. (1 Kor. 7:31) Zaidi ya hilo, watu wengi ambao wamejiunga na wahubiri wa habari njema ya Ufalme hawajafaidika na uchunguzi wa kitabu cha Ufunuo mustari kwa mustari. Kujifunza kitabu Ufunuo kutatusaidia sisi wote kubaki tukiwa macho kuhusu mambo yatakayotukia hivi karibuni.—Ufu. 16:15.

3 Azimia kuhuzuria funzo hilo kila juma. Habari hiyo itatusaidia si tu kuendelea kukesha lakini pia ujumbe mbalimbali ambao Yesu alitolea makutaniko saba utatusaidia kuepuka hali na mambo yanayoweza kuharibu hali yetu ya kiroho na kushiriki kwetu katika mahubiri.—Ufu. 1:11, 19.

4 Tayarisha Vizuri: Mbele ya kuhuzuria kila funzo la kitabu, soma katika Biblia maandiko ya kitabu cha Ufunuo ambayo yatachunguzwa. Andika mawazo ya Kimaandiko yanayofasiria andiko linalozungumziwa. Jikaze kuelewa mawazo makuu ili moyo wako uguswe. (Neh. 8:8, 12) Chukua wakati wa kutafakari (au kufikiri sana) na ujiulize: ‘Jambo hili linanifundisha nini kuhusu Yehova na kutimizwa kwa kusudi lake? Namna gani ninaweza kutenda kuhusiana na kusudi lake na kuwasaidia watu wengine?’

5 Miaka 92 imekwisha kupita tangu “siku ya Bwana” ilipoanza katika 1914. (Ufu. 1:10) Matukio ya ajabu yenye kutabiriwa katika kitabu cha Ufunuo yatatukia hivi karibuni. Kujifunza kitabu Ufunuo kutafurahisha mioyo yetu na kuchochea akili zetu, na kutatia nguvu imani yetu tunapojua kwamba “vita vya ile siku kuu ya Mungu Mweza-Yote” na ulimwengu mpya ni mambo yatakayotukia hivi karibuni.—Ufu. 16:14; 21:4, 5.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine