Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 10/07 uku. 1
  • Tolea Maskini Tumaini

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Tolea Maskini Tumaini
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2007
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Umasikini
    Amuka!—2015
Huduma Yetu ya Ufalme—2007
km 10/07 uku. 1

Tolea Maskini Tumaini

1 Yesu alihangaikia sana wale waliokuwa maskini. Wakati fulani fulani alitolea watu msaada wa kimwili na kuponyesha wagonjwa kwa njia ya miujiza, lakini jambo ambalo alikazia sana lilikuwa kutangazia maskini “habari njema.” (Mt. 11:5) Leo, maskini na watu wengine wanaendelea kufaidika kupitia kazi ya kuhubiri inayofanywa na Wakristo.—Mt. 24:14; 28:19, 20.

2 Tumaini la Kweli: Mara nyingi wahubiri wa dini zinazojiita za Kikristo wanaahidi maskini kwamba watapata mali nyingi ikiwa wanatolea kanisa kwa moyo wote. Lakini, Biblia inafundisha kwamba ni Ufalme wa Mungu tu ndio utamaliza umaskini na magumu yote ya wanadamu. (Zab. 9:18; 145:16; Isa. 65:21-23) Kwa kuonyesha maskini yale ambayo Biblia inafundisha kweli, tunawatolea tumaini na tunawasaidia watosheleze mahitaji yao ya kiroho.—Mt. 5:3.

3 Mafarisayo wa siku za Yesu walipuuza maskini kwa kuwaita kwa mazarau ‘am-ha·’aʹrets, ao “watu wa udongo.” Lakini, Yesu aliona “damu yao,” ao maisha yao kuwa yenye “thamani.” (Zab. 72:13, 14) Tunaweza kumwiga Yesu na ‘kuwaonyesha kibali’ maskini kama hao kwa kuwahangaikia wao na matatizo yao. (Met. 14:31) Hatupendi hata kidogo kusema kwa mazarau kuhusu watu wanaoishi katika maeneo ya watu walio maskini ao kusita kuwahubiria. Watu wengi wanaokubali kusikiliza habari ya Ufalme ni watu walio maskini.

4 Uwatolee Msaada Sasa: Kufundisha maskini kanuni za Biblia katika eneo letu kunawasaidia pia tangu sasa kupunguza mambo yanayotokeza umaskini. Kwa mfano, Biblia inakataza ulevi, michezo ya feza, uvivu, kuvuta tumbaku na vitendo vingine vinavyotokeza umaskini. (Met. 6:10, 11; 23:21; 2 Kor. 7:1; Efe. 5:5) Maandiko yanatia watu moyo kuwa wenye kufuatia haki na kufanya kazi “kwa nafsi yote,” sifa zinazohitajiwa kwa wafanyakazi. (Kol. 3:22, 23; Ebr. 13:18) Kwa hakika, katika uchunguzi mmoja uliofanywa, wakubwa wengi wa kazi walitoa mawazo yao wakisema kwamba walivutiwa sana na watu waliokuwa wakitafuta kazi ambao ni wenye kufuatia haki na waaminifu.

5 Yehova si mwenye kupuuza mateso ya maskini. Karibuni Yesu atakomboa “maskini anayelilia msaada.” (Zab. 72:12) Mpaka wakati huo, tuna nafasi ya pekee ya kutia wengine moyo, kutia ndani maskini, kupitia habari ya Biblia inayotoa tumaini.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine