Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 4/08 uku. 8
  • Fariji Wale Wenye Kuomboleza

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Fariji Wale Wenye Kuomboleza
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Habari za Kufanana na Zile
  • ‘Mulie Pamoja na Watu Wanaolia’
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2017
  • ‘Wafariji Wote Wanaoomboleza’
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Fariji Waliovunjika Moyo
    Huduma Yetu ya Ufalme—2007
Huduma Yetu ya Ufalme—2008
km 4/08 uku. 8

Fariji Wale Wenye Kuomboleza

1 Kufiwa na mtu tunayempenda ni jambo lenye kuhuzunisha sana, zaidi sana kwa wale wasio na tumaini la Ufalme. (1 The. 4:13) Wengi wanajiuliza maulizo kama haya: ‘Kwa nini watu wanakufa? Ni jambo gani linalowapata wanapokufa? Je, nitapata kumwona tena mtu ninayempenda aliyekufa?’ Hapa chini kuna mapendekezo fulani kuhusu jinsi ya kufariji wale tunaokutana nao katika kazi ya kuhubiri ambao wanaomboleza kifo cha mshiriki wa jamaa ao rafiki.—Isa. 61:2.

2 Unapohubiri Nyumba kwa Nyumba: Msikilizaji wetu anaweza kutuambia kwamba ametoka kupatwa na kifo katika jamaa. Je, ana huzuni nyingi ao ni mwenye kulia? Je, nyumba inajaa washiriki wa familia wenye kuomboleza? Katika hali hizo, si vizuri kubaki muda mrefu ili kutoa ushahidi. (Mhu. 3:1, 7) Labda tunaweza kumwonyesha kwamba tunasikitika kwa sababu ya jambo lililompata, kumtolea trakti, gazeti ao broshua inayoweza kumsaidia na kuondoka kwa heshima. Kisha tunaweza kumrudilia kwa wakati unaofaa ili kumfariji zaidi kutokana Biblia.

3 Nyakati nyingine, tunaweza kutambua kwamba tunaweza kusema mengi tunapokutana na mtu kwa mara ya kwanza. Hata ikiwa huo si wakati wa kupinga maoni yasiyo ya kweli, tunaweza kusoma na msikilizaji ahadi za Biblia kuhusu ufufuo. (Yoh. 5:28, 29) Ao tunaweza kumwonyesha yale ambayo Biblia inasema kuhusu hali ya wafu. (Mhu. 9:5, 10) Kumwelezea simulizi fulani la Biblia kuhusu ufufuo kunaweza pia kumfariji. (Yoh. 11:39-44) Njia ingine inaweza kuwa kuzungumzia maneno yaliyosemwa na mwaminifu Ayubu yenye kuonyesha tumaini alilokuwa nalo kwa Yehova. (Ayu. 14:14, 15) Mbele ya kuondoka tunaweza kumtolea broshua Jambo Gani Hutufikia Tunapokufa?, Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa..., ao broshua nyingine ao trakti inayofaa. Ao tunaweza kumwachia kitabu Biblia Inafundisha na kumwonyesha habari iliyo katika sura 6 na kupanga kuzungumzia zaidi habari hiyo tutakapomrudilia.

4 Kwenye Nafasi Nyingine: Ikiwa hotuba ya mazishi itafanywa kwenye Jumba la Ufalme, je, watu wasio Mashahidi watakuwa hapo? Tunaweza kutayarisha vitabu vinavyoweza kuwafariji. Katika mahali fulani, watu wenye kuomboleza wafu nyumbani, wanaweza kufurahia kupata vitabu fulani vinavyoweza kuwafariji. Nyakati fulani, matangazo ya vifo yanayotolewa katika gazeti la habari yanatoa nafasi ya kuandika barua fupi ya kuwafariji washiriki wa familia wanaoomboleza. Kwa mfano, mtu fulani aliyefiwa na mke wake alipopata barua iliyokuwa na trakti fulani ndani, yeye na binti yake walienda kwenye nyumba ya mhubiri na akauliza hivi: “Je, ni ninyi mulionitumia barua hii? Ninataka kujua mengi kuhusu Biblia!” Mtu huyo na binti yake walikubali kujifunza Biblia na wakaanza kuhuzuria mikutano ya kutaniko.

5 Andiko la Mhubiri 7:2 linasema hivi: “Ni afadhali kwenda katika nyumba ya maombolezo kuliko kwenda katika nyumba ya karamu.” Mara nyingi mtu mwenye kuomboleza ana mwelekeo mzuri wa kusikiliza Neno la Mungu kuliko yule aliye katika pindi la kujifurahisha. Sisi wote tunapaswa kuwa tayari kutambua nafasi zinazofaa ili kufariji wale wanaoomboleza kifo cha mtu wanayempenda.

[Maulizo ya Funzo]

1. Kwa nini wale wanaoomboleza wanahitaji kupata faraja?

2. Ikiwa msikilizaji wetu anatuambia kwamba ni mwenye kuomboleza, je, tubaki muda mrefu ili kumtolea ushahidi?

3. Ikiwa hali zinaruhusu, ni maandiko gani ambayo tunaweza kuonyesha msikilizaji wetu mwenye kuomboleza?

4. Tunaweza kuwafariji watu kwenye nafasi nyingine gani?

5. Kwa nini tunapaswa kutafuta nafasi za kufariji wale wanaoomboleza?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine