Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 7/10 uku. 1
  • Kazi ya Kutia pa Nafasi ya Kwanza

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kazi ya Kutia pa Nafasi ya Kwanza
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2010
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Unatimiza kwa Ukamili Utumishi Wako?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2019
  • Ni Jambo Gani Unalotanguliza?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • ‘Fuata Hatua Zake kwa Ukaribu’
    Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Huduma ya Kikristo—Kazi Yetu Kubwa
    Huduma Yetu ya Ufalme—2003
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2010
km 7/10 uku. 1

Kazi ya Kutia pa Nafasi ya Kwanza

1. Namna gani Yesu alionyesha kwamba kazi ya kuhubiri ilikuwa ya maana sana kwake?

1 Jambo ambalo Yesu alitia pa nafasi ya kwanza lilikuwa kazi ya kuhubiri. Alitumika sana, akitembea kilomita nyingi katika Palestina akihubiria watu wengi iwezekanavyo. Alifanya maisha yake yawe mepesi ili apate wakati mwingi wa kushugulikia kazi yake ya kuhubiri. (Mt. 8:20) Watu walipojaribu kumuzuia ili aendelee kuponyesha wagonjwa wao, yeye alisema: “Ni lazima nitangaze habari njema ya ufalme wa Mungu kwenye majiji mengine pia, kwa sababu nilitumwa kufanya hivyo.”—Luka 4:43.

2. Kwa nini kazi ya kuhubiri ilikuwa ya maana sana kwa Yesu?

2 Kwa nini kazi ya kuhubiri ilikuwa ya maana hivyo kwa Yesu? Hangaiko lake kubwa lilikuwa kutakasa jina la Yehova. (Mt. 6:9) Alimpenda Baba yake wa mbinguni, ni kwa sababu hiyo alipenda kutimiza mapenzi Yake na kutii kila amri Yake. (Yoh. 14:31) Zaidi ya hiyo, alihangaikia kabisa watu na alipenda kuwasaidia.—Mt. 9:36, 37.

3. Namna gani tutaonyesha kwamba kuhubiri ndilo jambo la maana sana kwetu?

3 Fuata Mfano wa Yesu: Kufanya kazi ya kuhubiri liwe jambo la kwanza la kuhangaikia kama Yesu si rahisi kwa kuwa ulimwengu unapenda kutuchukua wakati mwingi na unatutolea viburudisho vingi. (Mt. 24:37-39; Luka 21:34) Kwa hiyo, tunapaswa kujua mambo yaliyo ya maana zaidi, tukipanga wakati wa kujitayarisha na kushiriki katika kazi ya kuhubiri kwa ukawaida. (Flp. 1:10) Tunapaswa kujikaza kufanya maisha yetu yawe mepesi na kuepuka kutumia ulimwengu kwa ukamili.—1 Kor. 7:31.

4. Kwa nini ni jambo la maana kutia kazi ya kuhubiri pa nafasi ya kwanza?

4 Anapokuwa na wakati mchache, mutu mwenye hekima anafanya kwanza jambo ambalo ni la maana. Kwa mfano, anaposikia kwamba upepo mkali wenye hatari unakaribia, jambo la kwanza atakalofanya ni kutumia wakati wake na nguvu zake ili kutayarisha usalama wa familia yake na kujulisha majirani wake kuhusu hatari hiyo. Atafanya mambo mengine madogo-madogo nyuma. Wakati uliobaki mbele ya upepo mkali wa Har-magedoni kuanza umepungua. (Zef. 1:14-16; 1 Kor. 7:29) Ili tujiokoe na kuokoa wale wanaotusikiliza, tunapaswa kujiangalia sisi wenyewe na namna yetu ya kufundisha, iwe katika kutaniko ao inje ya kutaniko. (1 Tim. 4:16) Ndiyo, tutaokoka ikiwa tunatia pa nafasi ya kwanza kazi yetu ya kuhubiri!

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine