Je, Ninahubiri Vyakutosha?
1. Ni hali gani inayoweza kumuhangaisha Mkristo mwaminifu?
1 Je, umwekwisha kujiuliza ulizo hilo? Labda hauhubiri tena kama zamani kwa sababu ya uzee, matatizo ya afya, ao madaraka mengi ya familia, hilo linaweza kukuvunja moyo. Dada mmoja aliye na watoto watatu, aliandika kwamba wakati fulani alisumbuliwa kwa sababu wakati na nguvu ambazo angetumia ili kuhubiri alizitumia ili kuhangaikia familia yake. Ni nini itatusaidia tuwe na maoni yenye kusawazika?
2. Yehova anatutazamia tufanye nini?
2 Yehova Anatutazamia Tufanye Nini: Bila shaka, sisi wote tungependa kuhubiri zaidi. Lakini kuna tofauti kubwa kati ya yale ambayo tungependa kufanya na yale tunayoweza kufanya. Kwa kuwa tungependa kufanya mengi zaidi, hilo linamaanisha kwamba hatutosheke na yale tunayofanya. Tukumbuke kwamba Yehova anajua vizuri sana uwezo wetu na hatuombi tufanye zaidi ya yale tunayoweza kufanya. (Zab. 103:13, 14) Anatutazamia tufanye nini? Anapenda tumtumikie kwa nafsi yote, tumtolee utumishi ulio mzuri zaidi.—Kol. 3:23.
3. Namna gani kujua yale tunayoweza kufanya katika kazi ya kuhubiri?
3 Namna gani tutajua yale tunayoweza kufanya? Tunaweza kumwomba Yehova atusaidie tutende kulingana na hali yetu na uwezo wetu. (Zab. 26:2) Tunaweza kusaidiwa pia na rafiki yetu ambaye ni Mkristo aliyekomaa, anayetujua vizuri na ambaye anaweza kutuelezea bila kuogopa jambo tunalopaswa kufanya ili kutengeneza hali yetu. (Met. 27:9) Kumbuka pia kwamba kwa kuwa hali zinabadilika, ni jambo lenye kufaa kuchunguza hali yetu kwa ukawaida.—Efe. 5:10.
4. Namna gani tunapaswa kuona vikumbusho vya Kibiblia vinavyohusiana na kazi yetu ya kuhubiri?
4 Namna Tunavyopaswa Kuona Vikumbusho: Wakati wa shindano la mbio, watazamaji wanapaza sauti ili kutia moyo wakimbiaji. Wanafanya hivyo ili kusaidia wale wanaokimbia wafikie mradi wao, wasivunjike moyo. Hivyohivyo, vitia-moyo tunavyopata katika Biblia na vikumbusho vinavyotolewa kwenye mikutano yetu na katika vitabu vyetu vinavyotutia moyo ‘kuhubiri lile neno kwa bidii’ ni kwa faida yetu wala si kuonyesha kwamba bidii yetu ni ndogo. (2 Tim. 4:2) Tunaweza kuwa hakika kwamba tukiendelea kumtolea Yehova utumishi ulio mzuri zaidi, Yeye atakumbuka kabisa ‘upendo na kazi zetu.’—Ebr. 6:10.