Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 11/10 uku. 7
  • Ili Kuwa Wahubiri Wenye Bidii Ni Lazima Kutafakari

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Ili Kuwa Wahubiri Wenye Bidii Ni Lazima Kutafakari
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2010
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Uendelee Kutafakari Juu ya Mambo ya Kiroho
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Kutafakari
    Amuka!—2014
  • ‘Tumia Muzuri Zaidi Wakati Wako’
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2022
  • Mawazo ya Moyo Wangu
    ‘Tumuimbie Yehova kwa Furaha’
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2010
km 11/10 uku. 7

Ili Kuwa Wahubiri Wenye Bidii Ni Lazima Kutafakari

1. Ni nini kilichomsaidia Yesu asikengeushwe na kusahau kazi ya maana maishani mwake?

1 Yesu alipitisha mangaribi akiwaponya wagonjwa na kufukuza roho waovu. Wanafunzi wake walipomwona siku iliyofuata, walimwambia hivi: “Watu wote wanakutafuta,” na wakamwomba aendelee kuwaponya wagonjwa. Hata hivyo, Yesu hakukengeushwa na kusahau kazi ya maana maishani mwake, yaani kuhubiri habari njema. Alijibu hivi: “Twendeni mahali pengine, katika miji ya vijiji iliyo karibu, ili nipate kuhubiri huko pia, kwa maana nilitoka kwa kusudi hilo.” Ni nini kilichomsaidia Yesu aendelee kutia kazi ya kuhubiri pa nafasi ya kwanza? Aliamka asubuhi mapema ili kusali na kutafakari (ao kufikiri sana). (Marko 1:32-39) Namna gani kutafakari kunaweza kutusaidia sisi pia kuwa wahubiri wenye bidii?

2. Tunaweza kutafakari juu ya mambo gani ili tuendelee kuwa wahubiri wenye bidii?

2 Tutafakari Juu ya Mambo Gani? Yesu aliona kwamba watu walikuwa “wamechunwa ngozi na kutupwa huku na huku kama kondoo wasio na mchungaji.” (Mt. 9:36) Sisi pia, tunaweza kutafakari kuhusu jinsi watu wengi wanavyohitaji kusikia habari njema. Tunaweza kutafakari kuhusu uhitaji wa kutenda kwa haraka katika wakati ambamo tunaishi. (1 Kor. 7:29) Tunaweza kufikiri sana kuhusu kazi za Yehova na sifa zake, pendeleo letu la kuwa Mashahidi wa Yehova, na kuhusu mambo ya kiroho ya maana sana ambayo tumejifunza katika Neno la Mungu ambayo watu katika eneo letu hawajajua.​—Zab. 77:11-13; Isa. 43:10-12; Mt. 13:52.

3. Tunaweza kutafakari wakati gani?

3 Tutafakari Wakati Gani? Kama Yesu alivyofanya, watu fulani wanaamka asubuhi sana wakati kuna ukimya. Wengine wanaona vizuri zaidi kutafakari wakati wa mangaribi mbele ya kulala. (Mwa. 24:63) Hata ikiwa tuna mambo mengi ya kufanya, tunaweza kupata wakati wa kutafakari. Watu fulani wanatafakari wanapopatikana katika katika gari la watu wote, wakijielekeza mahali fulani. Wengine wanatumia wakati wa mapumziko ili watafakari bila kukengeushwa. Watu wengi wametambua kwamba kutafakari, hata kwa dakika chache, mbele ya kuenda katika mahubiri, kunawasaidia wahubiri kwa bidii na bila woga.

4. Kwa nini ni vizuri tutafakari?

4 Kutafakari kutatusaidia tuone ibada yetu kuwa jambo la maana zaidi katika maisha yetu, na kutatuchochea tukusudie sana kuendelea kuhubiri. Yesu, Mhubiri Mkuu wa Mungu, alipata faida kutokana na kutafakari, sisi pia tutafaidika ikiwa tunaendelea kutafakari.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine