Je, Watoto Wenu Wako Tayari?
1. Kwa nini watoto wanaokwenda kwenye masomo wanahitaji kutayarishwa?
1 Hivi karibuni mwaka mpya wa masomo utaanza. Bila shaka watoto wenu watakutana na magumu na mikazo mbalimbali. Watakuwa pia na nafasi mpya ya ‘kutoa ushahidi juu ya ile kweli.’ (Yoh. 18:37) Je, wako tayari?
2. Ili wawe tayari, watoto wenu wanapaswa kujua nini?
2 Je, watoto wako wanaelewa waziwazi kushiriki katika sherehe za kitaifa na sikukuu za kipagani kunamaanisha nini, na je, wanajua kwa nini si vizuri kushiriki katika sherehe hizo? Je, wako tayari kupambana na mikazo watakayokutana nayo kuhusu kufuatilia masomo ya juu, kufanya urafiki wa kimapenzi, na kutumia dawa zenye kulewesha? Je, wanasema tu kwamba ikiwa wanakataa jambo fulani ni kwa sababu dini yao inalikataza, ao wanajua jinsi ya kutetea imani yao?—1 Pet. 3:15.
3. Namna gani wazazi wanaweza kutumia Ibada ya Familia ya mangaribi ili kutayarisha watoto wao?
3 Mutumie Ibada ya Familia ya Mangaribi kwa Kuwatayarisha: Bila shaka, inaelekea kwamba mutakuwa na mazungumzo katika mwaka wote wa masomo kila wakati watoto wenu watakapopambana na magumu mbalimbali. Kujikaza kufikiria magumu wanayoweza kupata mbele hata ya kufungua masomo, hilo litawafanya watoto wenu wasiwe na woga. Kwa nini musitumie mangaribi moja ao zaidi ya Ibada yenu ya Familia ya mangaribi ili kuzungumzia magumu hayo? Munaweza kuuliza watoto wenu ni jambo gani linalowatia wasiwasi sana wanapofikiria kuanza mwaka mpya wa masomo. Mambo muliochunguza miaka iliyopita yanaweza tena kurudiliwa kwa kuwa sasa watoto wamekomaa na wameongeza uelewevu. (Zab. 119:95) Unaweza kupanga vipindi vya mazoezi ambamo utakuwa kama mwalimu, mshauri, ao mwanafunzi mwenzake. Mfundishe watoto wenu wajue jinsi ya kujibu kwa kutumia Biblia na vifaa kama vile kitabu Kutoa Sababu na Vijana Huuliza. Mzazi mmoja alitumia vipindi hivyo vya mazoezi ili kutayarisha watoto wake wakutane na walimu wao wapya mwanzoni mwa kila mwaka mpya wa masomo na kuwajulisha kwamba wao ni Mashahidi wa Yehova.—Ona Mnara wa Mlinzi wa tarehe 15 mwezi wa 12, 2010, ukurasa wa 3-5.
4. Wazazi wenye hekima watafanya nini?
4 Matatizo ambayo vijana Wakristo wanapambana nayo siku hizi za mwisho yanaendelea kuwa ‘ngumu kushugulika nayo.’ (2 Tim. 3:1) Wazazi wenye hekima watafikiria mbele ya wakati magumu ambayo watoto wao wanaweza kupata na wanawatayarisha ili kupambana nayo. (Met. 22:3) Mbele mwaka mpya wa masomo uanze, mufanye yote muwezayo ili kusaidia watoto wenu wawe tayari.