Sifa ya Maana Zaidi Inayomufanya Mutu Awe Mwalimu Muzuri
1. Ni sifa gani inayoweza kumufanya mutu awe mwalimu muzuri?
1 Ni nini inayoweza kumufanya mutu awe mwalimu muzuri wa Biblia? Je, ni masomo ya ulimwengu, kufanya siku nyingi katika kweli, ao uwezo fulani aliozaliwa nao? Kwa kweli, ni ile sifa inayotimiza Sheria, inayowatambulisha wafuasi wa kweli wa Yesu, na iliyo kubwa zaidi na yenye kuvutia kati ya sifa kubwa za Yehova. (Yoh. 13:35; Gal. 5:14; 1 Yoh. 4:8) Ni upendo. Walimu wazuri wanaonyesha upendo.
2. Kwa nini ni jambo la lazima tuwapende watu?
2 Tuwapende Watu: Yesu, Mwalimu Mukubwa, aliwapenda watu, na hilo liliwachochea wamusikilize. (Luka 5:12, 13; Yoh. 13:1; 15:13) Ikiwa kweli tunawahangaikia watu, tutatumia kila nafasi inayojitokeza ili kuwahubiria. Hatutaacha kuhubiri hata ikiwa watu wanatupinga ao hawapendezwi. Tutaonyesha kwamba tunapendezwa kabisa na watu tunaohubiria, na tutapatanisha mazungumuzo yetu na mambo yanayowasumbua ao yanayowapendeza. Tutafikiria hali ya kila mwanafunzi si wakati wa funzo tu lakini pia tunapotayarisha habari ya kujifunza naye.
3. Kupenda mambo ambayo Biblia inafundisha kutatusaidia namna gani katika mahubiri?
3 Tupende Mambo Ambayo Biblia Inafundisha: Yesu alipenda mambo ambayo Biblia inafundisha na aliyaona kuwa ya maana sana. (Mt. 13:52) Ikiwa tunapenda kweli, tutazungumuza na watu kwa uchangamufu, na hilo linaweza kuwachochea wasikilize. Upendo kama huo utatusaidia tukazie akili zetu juu ya habari ya maana tunayohubiria watu kuliko kukazia akili juu ya uzaifu tulio nao, na jambo hilo linaweza kutusaidia tupunguze wasiwasi tulio nao tunapohubiri.
4. Tunaweza kufanya nini ili tukomalishe upendo wetu?
4 Tukomalishe Upendo Wetu: Tunaweza kufanya nini ili tukomalishe upendo wetu? Tufikirie upendo ambao Yehova na Mwana wake wameonyesha na pia tufikirie hali mbaya ya kiroho ya watu wa eneo letu. (Marko 6:34; 1 Yoh. 4:10, 11) Kufanya funzo la pekee kwa ukawaida na kufikiri sana kuhusu mambo tunayojifunza kutatusaidia tupende zaidi mambo ambayo Biblia inafundisha. Upendo ni sehemu ya tunda la roho. (Gal. 5:22) Kwa hiyo, tunaweza kumwomba Yehova roho yake na kumwomba atusaidia tukomalishe upendo wetu. (Luka 11:13; 1 Yoh. 5:14) Kuonyesha upendo ndiko kutatusaidia tuwe walimu wazuri, si masomo tuliyosoma, si siku nyingi tulizofanya katika kweli, wala uwezo tuliozaliwa nao.