Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 1/14 uku. 1
  • Tuige Mufano wa Manabii​—Mika

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Tuige Mufano wa Manabii​—Mika
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2014
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Endelea Kuonyesha ‘Mutazamo wa Kungojea’
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
Huduma Yetu ya Ufalme—2014
km 1/14 uku. 1

Tuige Mufano wa Manabii​—Mika

1. Sababu gani tunapaswa kuamini kwamba ulimwengu huu mwovu utaharibiwa wakati ambao Yehova amepanga?

1 Alipokuwa akitangaza hukumu ya Yehova juu ya Israeli na Yuda, pengine nabii Mika alijiuliza ulizo hili: ‘Mwisho wa ulimwengu huu mwovu utafika wakati gani?’ Hata hivyo, aliamini kwamba mambo aliyotabiri yatatimia. Katika mwaka wa 740, Mika alijionea hukumu ya Yehova ikitimia juu ya Samaria. (Mika 1:6, 7) Kisha, katika mwaka wa 607, muji wa Yerusalemu uliharibiwa. (Mika 3:12) Leo, sisi pia tunangojea hukumu ya Yehova. Namna gani tunaweza kumuiga nabii Mika?

2. Sababu gani tunapaswa kuwa wavumilivu tunapongojea siku ya Yehova na namna gani tutaonyesha sifa hiyo?

2 Tuonyeshe Uvumilivu: Nabii Mika aliandika hivi: ‘Mimi, nitaendelea kumutazamia Yehova. Nitaonyesha mutazamo wa kumungojea Mungu wa wokovu wangu.’ (Mika 7:7) Kwa kweli, Mika hakukaa tu na kungojea mwisho bila kufanya jambo lolote. Aliendelea kutoa unabii kwa bidii. Leo, tunaendelea kungojea siku ya Yehova; kwa hiyo ni lazima tuwe na bidii katika ‘matendo matakatifu ya mwenendo na vitendo vya kushikamana na Mungu.’ (2 Pet. 3:11, 12) Yehova halete siku hiyo haraka kwa sababu Yeye ni muvumilivu. Uvumilivu huo unawatolea watu nafasi ya kutubu. (2 Pet. 3:9) Kwa hiyo, tunachukua kwa uzito shauri la Biblia la kuiga uvumilivu wa manabii.​—Yak. 5:10.

3. Sababu gani tumuombe Yehova atupe roho yake?

3 Tutegemee Nguvu ya Yehova: Mika alikuwa na mugawo mugumu; kwa hiyo alitegemea nguvu ya Yehova ili kuutimiza. (Mika 3:8) Mungu anajua kwamba tunahitaji nguvu kutoka kwake, kwa hiyo anatutia moyo tumuombe atupe nguvu. Kwa ukarimu, Yehova anawapa nguvu wale wenye kuchoka ili watimize madaraka yao ya kiteokrasi. (Zab. 84:5, 7; Isa. 40:28-31) Umekwisha kujionea jambo fulani lililokusadikisha kwamba Yehova anakupa nguvu katika utumishi mutakatifu unaomutolea? Unaendelea kumuomba Yehova roho yake takatifu bila kuchoka?​—Lu. 11:13.

4. Namna gani tunaonyesha kila siku kwamba Yehova ni Mungu wetu?

4 Nabii Mika alitia mapenzi ya Mungu pa nafasi ya kwanza katika maisha yake. Aliendelea kuwa mwaminifu hata kama alizungukwa na watu wenye mwenendo muchafu. Sisi pia, tunajaribiwa kila siku. Acheni basi tuendelee hata zaidi ‘kutembea katika jina la Yehova milele na milele.’​—Mika 4:5.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine