Kisanduku Cha Maulizo
◼ Ni Mambo gani watoto wanapashwa kujifunza ili wakomae kiroho?
Wazazi Wakristo wanafanya yote wanayoweza ili kuwalea watoto wao ‘katika nizamu na muongozo wa akilini wa Yehova.’ (Efe. 6:4; ona maelezo ya chini katika Rbi8-F.) Kwa mufano, wazazi wameona kwamba ni jambo la lazima kuchunguza andiko la siku kila asubuhi pamoja na watoto wao. Wakati wa ibada ya familia na wakati mwengine, wanaweza kutazama na kuzungumuzia video fulani pamoja, kuzungumuzia habari fulani katika kitabu Vijana Huuliza inayopatana na mahitaji ya familia yao, kucheza hadisi fulani za Biblia, ao kufanya vipindi vya mazoezi. Ili watoto ‘waelekee kwenye [ao wafikie] ukomavu,’ wanapashwa pia kufundishwa mafundisho mazito ya Biblia.—Ebr. 6:1.
Fikiria yale tunayofundisha watu tunaokutana nao katika eneo letu. Tunapowatembelea kwa mara ya kwanza ao tunapowarudilia, mara nyingi tunajikaza kuanzisha funzo la Biblia kwa kutumia kitabu Biblia Inafundisha Kabisa Nini? Kisha kumaliza kitabu hicho, tunatumia kitabu Mubaki “Katika Upendo wa Mungu.” Sababu gani? Kwa sababu kitabu Biblia Inafundisha kinawasaidia wanafunzi kuwa na ujuzi wa musingi wa Maandiko. Kitabu “Upendo wa Mungu” kinawafundisha namna ya kutumikisha kanuni za Biblia katika maisha yao ya kila siku. Kujifunza vitabu hivyo viwili kunawasaidia wapya wawe na “mizizi” katika Kristo na ‘wawe imara katika imani.’ (Kol. 2:6, 7) Vitabu hivyo vinaweza pia kuwasaidia watoto wetu. Tunapashwa kuwafundisha kuhusu zabihu ya ukombozi, Ufalme, na hali ya watu waliokufa. Watoto wanahitaji pia kujua sababu gani Mungu anawaacha watu wateseke na namna ya kutambua siku za mwisho za ulimwengu huu muovu. Wanapashwa kusadikishwa kwamba Mashahidi wa Yehova wanafundisha kweli. Vijana hao wanapashwa pia kuelewa kanuni za Biblia na namna ya kuzoeza “nguvu zao za ufahamu.” (Ebr. 5:14) Lakini, wazazi wanapashwa kufikiria miaka na mambo yenye watoto wao wanaweza kuelewa. Hata hivyo, watoto wengi wanaweza kuwa na uwezo wa kuelewa mafundisho mazito ya Biblia hata kama wangali wadogo.—Luka 2:42, 46, 47.
Ili kuwasaidia wazazi, misaada ya kujifunza inayotegemea kitabu Biblia Inafundisha itapatikana kwenye adresi yetu ya Internete jw.org. Familia zinaweza kupata habari hizo kwenye adresi yetu kwa kufungua MAFUNDISHO YA BIBLIA > VIJANA. Wakati unaokuja, habari zingine zinazotegemea kitabu “Upendo wa Mungu” zitapatikana kwenye adresi yetu ya Internete. Hata hivyo, vichapo hivyo vyenye vimekwisha kuchapishwa vinaweza kutumiwa. Wazazi wanaweza kuamua ikiwa watatumia habari hizo katika sehemu ya Ibada yao ya Familia ya mangaribi, wanapojifunza na mutoto mumoja-mumoja ao wanapomuzoeza mutoto kufanya funzo lake la pekee.