Utaiga Bidii ya Yehova na ya Yesu Katika Kipindi Hiki cha Ukumbusho?
1. Katika kipindi cha Ukumbusho Mashahidi wa Yehova wanafanya mupango gani wa pekee?
1 Yehova anatimiza kusudi lake kwa bidii. Andiko la Isaya 9:7 linasema hivi kuhusu baraka fulani za Ufalme wa Mungu: “Bidii ya Yehova wa majeshi itafanya hayo.” Wakati alikuwa hapa duniani, Mwana wa Mungu pia alionyesha bidii kubwa kwa ajili ya ibada ya kweli. (Yohana 2:13-17; 4:34) Kila mwaka, katika kipindi cha Ukumbusho, wahubiri wengi duniani kote wanafanya mupango wa pekee kwa kuongeza bidii katika mahubiri ili kuiga bidii ya Yehova na ya Yesu. Utafanya hivyo pia?
2. Bidii itatuchochea kufanya nini kuanzia tarehe 7 Mwezi wa 3?
2 Kampanye ya Ukumbusho: Mwaka huu, kampanye ya kualika watu kwenye Ukumbusho itaanza Siku ya Posho, tarehe 7 Mwezi wa 3. Jitayarishe tangu sasa ili kuhubiri kwa bidii. Makutaniko yatachangamuka sana wakati wahubiri watatolea watu mialiko katika eneo lote la kutaniko lao kadiri inawezekana. Tufanye yetu yote ili kuwaalika wanafunzi wetu wa Biblia, watu wenye tunarudilia, wafanya-kazi wenzetu, watu wa jamaa, na wanafunzi wenzetu kwa kuwapatia mialiko ao kwa kutumia jw.org.
3. Namna gani tunaweza kuongeza utumishi wetu katika Mwezi wa 3 na wa 4?
3 Upainia Musaidizi: Bidii itatuchochea pia kuongeza utumishi wetu. Bila shaka wahubiri wengi watakuwa mapainia wasaidizi katika Mwezi wa 3 na wa 4, kwa sababu itawezekana kwetu kuwa mapainia wa saa 30. Wakati wa ibada yenu ya familia, ao wakati wa funzo la pekee, muchunguze namna ya kufanya hivyo na musali kwa ajili ya hilo. (Met. 15:22) Bidii yako kwa ajili ya kampanye hii inaweza kuwachoche wengine pia wakuwe na bidii. Ikiwa unapanga programu yako ili kuhubiri sana, utakuwa unaiga bidii ya Yesu.—Mk. 6:31-34.
4. Tutapata baraka gani kwa kuiga bidii ya Yehova na ya Yesu?
4 Tutapata baraka nyingi kama tutaiga bidii ya Yehova na ya Yesu katika kipindi hiki cha Ukumbusho. Watu wengi zaidi watahubiriwa katika eneo. Tutatosheka na kupata furaha yenye inatokana na kutoa na kumutumikia Yehova. (Mdo. 20:35) Zaidi sana, tutafurahisha moyo wa Mungu wetu na Mwana wake ambao ni wenye bidii.