UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | ESTA 6-10
Esta Alijitoa kwa Ajili ya Yehova na Watu Wake
Esta alikuwa na ujasiri na alijinyima ili kumutetea Yehova na watu wake
Esta na Mordekai hawakuwa katika hatari. Lakini sheria ya Hamani ya kuwaua Wayahudi wote ilitolewa katika utawala wote
Esta alihatarisha tena uzima wake, kwa kuenda mbele ya mufalme pasipo kualikwa. Alilia kwa ajili ya watu wa taifa lake na kuomba mufalme avunje sheria kali yenye ilitolewa
Sheria zenye zilitolewa kupitia jina la mufalme hazingevunjwa. Kwa hiyo, mufalme alipatia Esta na Mordekai mamulaka ya kuandika sheria mupya
Yehova aliwapatia watu wake ushindi mukubwa
Tangazo la pili lilitolewa, lenye kuwapa Wayahudi haki ya kujilinda ili wasishambuliwe
Wapanda-farasi walienda mbio katika sehemu zote za utawala, na Wayahudi walijitayarisha kwa ajili ya vita
Watu wengi walitambua kwamba Mungu alikuwa pamoja na watu wake na waliamini na kujiunga na dini ya Kiyahudi