Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • wp20 na. 3 uku. 11
  • Tunapaswa Kumutii Mungu juu Tupate Baraka

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Tunapaswa Kumutii Mungu juu Tupate Baraka
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2020
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • 1. WAKATI TUNAMUTII MUNGU, TUNAKUWA NA HEKIMA
  • 2. WAKATI TUNAMUTII MUNGU, TUNAKUWA NA FURAHA
  • Upendo wa Mungu Hauna Mwisho
    Namna ya Kubakia Katika Upendo wa Mungu
  • ‘Kumupenda Mungu Kunamaanisha Hivi’
    Mubaki “Katika Upendo wa Mungu”
  • Uko “Tayari Kutii”?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2023
  • “Mimi Niko Mahali pa Mungu?”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2020
wp20 na. 3 uku. 11
Familia inapitisha wakati pamoja kwa furaha. Mama anapika chakula pamoja na mutoto wake mumoja mwanamuke. Baba iko anaangalia picha pamoja na mutoto mwingine mwanamuke.

Tunaweza kupata furaha ya kweli kwa kutii amri za Mungu

Tunapaswa Kumutii Mungu juu Tupate Baraka

Nabii Musa alisema kama ikiwa tunatii amri za Mungu, tutapata baraka za Mungu. (Kumbukumbu la Torati 10:13; 11:27) Hatumutii Mungu juu ya kuogopa malipizi. Sifa za Mungu zinatuchochea tumutii juu tunamupenda na tunataka kuepuka kufanya jambo lenye linaweza kumuhuzunisha. Neno la Mungu linasema: “Kumupenda Mungu kunamaanisha hivi, kwamba tushike amri zake.”​—1 Yohana 5:3.

Namna gani kumutii Mungu kunatuletea baraka? Tufikirie njia mbili.

1. WAKATI TUNAMUTII MUNGU, TUNAKUWA NA HEKIMA

“Mimi, Yehova, niko Mungu wako, Mwenye anakufundisha ili ujipatie faida, Mwenye anakuongoza katika njia yenye unapaswa kutembea ndani yake.”​—ISAYA 48:17.

Yehova Mungu, Muumbaji wetu, anatujua na anatutolea muongozo wenye tuko nao lazima. Kama tunapenda mafundisho yake itusaidie kukamata maamuzi ya hekima, tunapaswa kujifunza Maandiko Matakatifu juu tujue mambo yenye anapenda tufanye na kisha tunapaswa kuifanya.

2. WAKATI TUNAMUTII MUNGU, TUNAKUWA NA FURAHA

“Wenye furaha ni wale wenye wanasikia neno la Mungu na kulishika!”​—LUKA 11:28.

Leo, mamilioni ya watu wenye wanatii Neno la Mungu wanapata furaha ya kweli. Kwa mufano, fikiria mwanaume mumoja wa Espagne mwenye alikuwa na tabia ya kukasirika haraka na ya kutendea wengine kwa ukali, na hata bibi yake. Siku moja alisoma mambo yenye nabii Musa aliandika kuhusu sifa ya upole ya Yosefu, mwana wa Yakobo. Yosefu aliuzishwa katika utumwa na alifungwa hata kama hakufanya kosa; lakini aliendelea kuwa mupole, mwenye kupenda amani, na mwenye kusamehe. (Mwanzo, sura ya 37-45) Ule mwanaume wa Espagne alisema: “Kufikiri kuhusu mufano wa Yosefu kulinisaidia nikuwe na sifa ya upole, wema, na kujizuia. Na sasa niko na furaha.”

Maandiko inatupatia mashauri zaidi kuhusu namna tunapaswa kutendea wengine. Fikiria ile mashauri mu habari yenye kufuata.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine