Kuhubiri nyumba kwa nyumba katika Italie
Namna ya Kuanzisha Mazungumuzo
MUNARA WA MULINZI
Ulizo: Unawaza Mungu alituumba ili tukufe?
Andiko: Ufu 21:4
Namna ya kutoa: Hii gazeti Munara wa Mulinzi inazungumuzia mambo Biblia inasema juu ya kifo.
FUNDISHA KWELI
NAMNA GANI TUNAJIFUNZA BIBLIA NA WATU?
Tunaweza kusema: Mashahidi wa Yehova wanajifunza Biblia na watu kwa bure ili kuwasaidia kupata majibu ya maulizo kama vile: Sababu gani tunateseka sana? Namna gani familia yangu inaweza kuwa na furaha? Video hii ya mufupi inaonyesha namna tunajifunza Biblia na watu. [Onyesha video Tunajifunzaka Biblia na watu Namna Gani?] Tunaweza kujifunza Biblia kupitia kitabu hiki. [Onyesha moja kati ya vitabu ao broshua zenye tunatumia ili kujifunza Biblia na watu.]
ANDIKA NAMNA UNAWEZA PIA KUANZISHA MAZUNGUMUZO
Fuata mufano wenye kuwa hapo juu ili kuandika namna yako ya kuanzisha mazungumuzo.