Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • mwb17 Mwezi wa 10 uku. 3
  • Namna Gani Unaweza Kuwa Mwanafunzi Muzuri wa Maandiko?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Namna Gani Unaweza Kuwa Mwanafunzi Muzuri wa Maandiko?
  • Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2017
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Je, Kweli Mungu Anakujali?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Ujifunze kwa Undani juu Uendelee Kuwa Macho
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
  • Unaendelea Kumutumikia Yehova?
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2017
  • Tujifunze Mambo Fulani Kupitia Mufano wa Danieli
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2023
Ona Habari Zaidi
Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2017
mwb17 Mwezi wa 10 uku. 3

MAISHA YA MUKRISTO

Namna Gani Unaweza Kuwa Mwanafunzi Muzuri wa Maandiko?

Wakati wa majaribu, ungependa kuwa muaminifu kama Danieli? Danieli alijifunza Neno la Mungu kwa uangalifu, hata unabii wenye ulikuwa nguvu sana kuelewa. (Dan 9:2) Kujifunza Biblia kwa uangalifu kunaweza kukusaidia uendelee kuwa muaminifu. Namna gani? Kunaweza kukufanya ukuwe na imani zaidi kama ahadi zote za Yehova zitatimia. (Yos 23:14) Kunaweza pia kukusaidia umupende Mungu zaidi, na hilo litakuchochea kufanya mambo ya muzuri. (Zab 97:10) Lakini, utaanzia wapi? Tuchunguze mapendekezo fulani.

Danieli anajifunza Neno la Mungu
  • Nijifunze Nini? Kama uko mwanafunzi muzuri wa Maandiko, unapaswa kutayarisha mikutano ya kutaniko. Usomaji wa Biblia wa kila juma utakuletea faida kabisa kama unachukua wakati wa kutafuta mambo yenye hauelewe. Tena, watu fulani wamechagua kujifunza mengi zaidi juu ya unabii wa Biblia, sehemu mbalimbali za tunda la roho takatifu ya Mungu, safari za umisionere za mutume Paulo, ao vitu vyenye Yehova aliumba. Kama unajiuliza ulizo fulani juu ya Biblia, uliandike ili utafute jibu wakati wako wa funzo.

  • Nitafute wapi habari za kujifunza? Ili kupata mapendekezo fulani, angalia video Vyombo vya Kutusaidia Kutafuta Mali ya Kiroho. Kwa mufano, tafuta kujua serikali kubwa za ulimwengu zenye kufananishwa na wanyama wenye kuzungumuziwa katika sura ya 7 ya Danieli.

  • Nijifunze kwa saa ngapi? Kujifunza kwa ukawaida kunasaidia kuwa na afya muzuri ya kiroho. Unaweza kuanza kwa vipindi vifupi-vifupi, kisha unaweza kuongeza urefu polepole. Kujifunza Neno la Mungu ni kama kuchimba ili kutafuta mali fulani yenye kufichwa; kadiri utaendelea kuipata ni vile utakuwa na hamu ya kuchimba tena! (Met 2:3-6) Tamaa yako ya kujifunza Neno la Mungu itaongezeka, na kujifunza Biblia kwa ukawaida kutakuwa sehemu ya maisha yako.—1Pet 2:2.

    Amuka! ya Mwezi wa 2, 2012, ukurasa wa 18-20 inatoa mapendekezo mengine juu ya namna ya kufanya funzo likuwe lenye kupendeza.

WANYAMA WENYE KUZUNGUMUZIWA KATIKA SURA YA 7 YA DANIELI WANAFANANISHA NINI?

  • Munyama wa mabawa ya tai mwenye kufanana na simba

    Dan 7:4

  • Munyama mwenye kufanana na dubu anabeba mbavu katika kinywa chake

    Dan 7:5

  • Munyama wa vichwa ine na mabawa ine mwenye kufanana na chui

    Dan 7:6

  • Munyama wa meno murefu ya chuma na pembe kumi mwenye kuogopesha sana

    Dan 7:7

ULIZO LINGINE:

Danieli 7:8, 24 ilitimia namna gani?

Pembe kidogo lenye kuwa na macho na kinywa linaota katikati ya pembe kumi, kisha linachukua nafasi ya pembe tatu

YA SIKU INGINE

Wanyama wenye kuzungumuziwa katika sura ya 13 ya Ufunuo wanafananisha nini?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine