MAISHA YA MUKRISTO
Namna Gani Unaweza Kuwa Mwanafunzi Muzuri wa Maandiko?
Wakati wa majaribu, ungependa kuwa muaminifu kama Danieli? Danieli alijifunza Neno la Mungu kwa uangalifu, hata unabii wenye ulikuwa nguvu sana kuelewa. (Dan 9:2) Kujifunza Biblia kwa uangalifu kunaweza kukusaidia uendelee kuwa muaminifu. Namna gani? Kunaweza kukufanya ukuwe na imani zaidi kama ahadi zote za Yehova zitatimia. (Yos 23:14) Kunaweza pia kukusaidia umupende Mungu zaidi, na hilo litakuchochea kufanya mambo ya muzuri. (Zab 97:10) Lakini, utaanzia wapi? Tuchunguze mapendekezo fulani.
Nijifunze Nini? Kama uko mwanafunzi muzuri wa Maandiko, unapaswa kutayarisha mikutano ya kutaniko. Usomaji wa Biblia wa kila juma utakuletea faida kabisa kama unachukua wakati wa kutafuta mambo yenye hauelewe. Tena, watu fulani wamechagua kujifunza mengi zaidi juu ya unabii wa Biblia, sehemu mbalimbali za tunda la roho takatifu ya Mungu, safari za umisionere za mutume Paulo, ao vitu vyenye Yehova aliumba. Kama unajiuliza ulizo fulani juu ya Biblia, uliandike ili utafute jibu wakati wako wa funzo.
Nitafute wapi habari za kujifunza? Ili kupata mapendekezo fulani, angalia video Vyombo vya Kutusaidia Kutafuta Mali ya Kiroho. Kwa mufano, tafuta kujua serikali kubwa za ulimwengu zenye kufananishwa na wanyama wenye kuzungumuziwa katika sura ya 7 ya Danieli.
Nijifunze kwa saa ngapi? Kujifunza kwa ukawaida kunasaidia kuwa na afya muzuri ya kiroho. Unaweza kuanza kwa vipindi vifupi-vifupi, kisha unaweza kuongeza urefu polepole. Kujifunza Neno la Mungu ni kama kuchimba ili kutafuta mali fulani yenye kufichwa; kadiri utaendelea kuipata ni vile utakuwa na hamu ya kuchimba tena! (Met 2:3-6) Tamaa yako ya kujifunza Neno la Mungu itaongezeka, na kujifunza Biblia kwa ukawaida kutakuwa sehemu ya maisha yako.—1Pet 2:2.
WANYAMA WENYE KUZUNGUMUZIWA KATIKA SURA YA 7 YA DANIELI WANAFANANISHA NINI?
Dan 7:4
Dan 7:5
Dan 7:6
Dan 7:7
ULIZO LINGINE:
Danieli 7:8, 24 ilitimia namna gani?
YA SIKU INGINE
Wanyama wenye kuzungumuziwa katika sura ya 13 ya Ufunuo wanafananisha nini?