Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • mwb18 Mwezi wa 4 uku. 8
  • Ili Kufanya Wanafunzi, Tunapaswa Kuhubiri na Kufundisha

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Ili Kufanya Wanafunzi, Tunapaswa Kuhubiri na Kufundisha
  • Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2018
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Tukomalishe Ufundi Wetu wa Kuhubiri—Tusaidie Wale Wenye Kuwa na ‘Muelekeo Wenye Kufaa’ Wakuwe Wanafunzi
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2018
  • Unaweza Kusaidia mu Kazi ya Kufanya Wanafunzi?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2021
  • Tutangaze Bila Kuacha Habari Njema
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • ‘Muende Mufanye Wanafunzi Kutoka kwa Watu wa Mataifa Yote’
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2016
Ona Habari Zaidi
Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2018
mwb18 Mwezi wa 4 uku. 8

MAISHA YA MUKRISTO

Ili Kufanya Wanafunzi, Tunapaswa Kuhubiri na Kufundisha

Yesu aliamuru wafuasi wake waende na wafanye wanafunzi. (Mt 28:19) Ili kufanya hivyo inaomba kuhubiri na kufundisha. Mara kwa mara, tunapaswa kujiuliza hivi: ‘Namna gani ninaweza kufanya maendeleo katika sehemu hizi mbili za maana sana za kazi ya kufanya wanafunzi?’

KUHUBIRI

Kuliko kungojea watu wakuje kwetu, tunapaswa kutafuta kwa bidii watu wenye ‘kustahili’. (Mt 10:11) Wakati tunahubiri, tunatafuta nafasi za kuzungumuza na watu wote wenye tunakutana nao? (Mdo 17:17) Mutume Paulo alihubiri kwa bidii, na hilo lilifanya Lidia afikie kuwa mwanafunzi.​—Mdo 16:13-15.

Samuel anamutolea Ezekiel gazeti; Salomon na Marie wanahubiria Ezekiel na Abigail

‘Asubuhi panda mbegu zako na mupaka jioni usiache mukono wako upumuzike’ (Mhu 11:6)

MUANGALIE VIDEO ZENYE VICHWA ENDELEA KUHUBIRI “BILA KUACHA”​—MAHUBIRI YENYE HAYAKUPANGWA NA YA NYUMBA KWA NYUMBA, KISHA MUJIBIE MAULIZO HAYA:

  • Wakati alikuwa anafanya kazi yake ya kila siku, namna gani Samuel alionyesha kama alitafuta kwa bidii kupanda mbegu za ukweli?

  • Sababu gani tunapaswa kuendelea kushiriki katika sehemu zote za mahubiri?

  • Wakati unafanya kazi yako ya kila siku, unaweza kuhubiria nani habari njema ya Ufalme?

KUFUNDISHA

Ili kufanya wanafunzi, haitoshe tu kuachia watu vichapo. Ili kuwasaidia waendelee kiroho, tunapaswa kuwarudilia na kujifunza nao Biblia. (1Kor 3:6-9) Sasa, tutafanya nini kama tunajikaza kufundisha mutu fulani kweli ya Ufalme, lakini hafanye maendeleo? (Mt 13:19-22) Tunapaswa kuendelea kutafuta wale wenye mioyo yenye kuwa kama ‘udongo muzuri.’​—Mt 13:23; Mdo 13:48.

Salomon na Marie wanajifunza Biblia na Ezekiel na Abigail; Ezekiel na Abigail wanahubiri mahali pa watu wengi

“Mimi nilipanda, Apolo akatia maji, lakini Mungu akaendelea kuikuza [kuikomalisha]” (1Kor 3:6)

MUANGALIE VIDEO ZENYE VICHWA ENDELEA KUHUBIRI “BILA KUACHA”​—MAHALI PA WATU WENGI NA KUFANYA WANAFUNZI, KISHA MUJIBIE MAULIZO HAYA:

  • Namna gani Salomon na Marie walimuangia maji mbegu za ukweli zenye zilipandwa katika moyo wa Ezekiel na Abigail?

  • Tunapaswa kuwa na muradi gani wakati tunashiriki katika sehemu zote za mahubiri, hata wakati tunahubiri mahali pa watu wengi?

  • Namna gani tunaweza kukazia sana kufundisha wengine kweli?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine