MAISHA YA MUKRISTO
“Kile Chenye Mungu Ameunganisha . . .”
Sheria ya Musa ilimuomba mwanaume mwenye alifikiria kuvunja ndoa atayarishe cheti cha kuvunja ndoa chenye kukubaliwa na sheria. Mupango huo ulifanya watu wasiamue haraka-haraka kuvunja ndoa. Lakini, wakati Yesu alikuwa katika dunia, viongozi wa dini walifanya ikuwe mwepesi sana kuvunja ndoa. Wanaume walivunja ndoa kwa sababu yoyote. (“cheti cha kuvunja ndoa”, kwa ajili ya funzo kuhusu Mk 10:4, nwtsty-E; “kuvunja ndoa na muke wake”, “anafanya uzinzi zidi yake” kwa ajili ya funzo Mk 10:11, nwtsty-E) Yesu aliwakumbusha kama ni Yehova aliruhusu mupango wa ndoa na kuuanzisha. (Mk 10:2-12) Bibi na bwana wanapaswa kuwa “mwili moja” na kuendelea kuishi pamoja. Kulingana na kitabu cha Mathayo, sababu moja tu yenye kukubaliwa na Maandiko ya kuvunja ndoa ni “uasherati.”—Mt 19:9.
Leo, watu wengi hawaone ndoa kama vile Yesu aliiona, lakini wanaiona kama vile Mafarisayo waliiona. Wakati magumu inatokea, watu wa ulimwengu wanakimbilia kuvunja ndoa. Lakini, Bibi na bwana Wakristo wanakamata naziri yao ya ndoa kwa uzito na wanajikaza kumaliza matatizo yao kwa kutumikisha kanuni za Biblia. Kisha kuangalia video Kuwa na Upendo na Heshima Kunaunganisha Familia, mujibie maulizo haya:
Namna gani unaweza kutumia Methali 15:1 katika ndoa yako, na sababu gani ni jambo la maana?
Kama unatumikisha Methali 19:11, namna gani unaweza kuepuka matatizo?
Kama ndoa yako inataka kuvunjika, kuliko kukimbilia kuivunja, unapaswa kujiuliza maulizo gani?
Kama unatumikisha Mathayo 7:12, namna gani unaweza kuwa bwana ao bibi muzuri?