MAISHA YA MUKRISTO
Mukumbuke Bibi ya Loti
Sababu gani bibi ya Loti aliangalia nyuma wakati alikuwa anakimbia Sodoma? Biblia haiseme. (Mwa 19:17, 26) Lakini onyo la Yesu linaonyesha kama pengine alitamani vitu vyenye aliacha nyuma. (Lu 17:31, 32) Bibi ya Loti alipoteza pendeleo la kukubaliwa na Mungu; namna gani tunaweza kuepuka kumuiga? Hatupaswe kuruhusu kutafuta vitu vya kimwili kuchukue nafasi ya kwanza katika maisha yetu. (Mt 6:33) Yesu alifundisha kama ‘hatuwezi kuwa watumwa wa Mungu na wa Utajiri.’ (Mt 6:24) Lakini, tukivumbula kama vitu vya kimwili vimeanza kuchukua wakati wenye tunapaswa kutumia kwa ajili ya mambo ya kiroho, tutafanya nini? Tunaweza kumuomba Yehova atupatie utambuzi ili kuona mahali tunapaswa kufanya mabadiliko, na kumuomba atupatie ujasiri na nguvu ya kufanya mabadiliko hayo.
KUMBUKA VIDEO YENYE SEHEMU TATU MUKUMBUKE BIBI YA LOTI, KISHA MUJIBIE MAULIZO YENYE KUFUATA:
Namna gani ninaweza kuonyesha kupitia matendo yangu kama “ninakumbuka bibi ya Loti”?
Wakati Gloria alichochewa kutafuta kupata feza mingi, hilo lilikuwa na matokeo gani juu ya mawazo, maneno, na matendo yake?
Namna gani mufano wa bibi ya Loti ni onyo kwetu leo?
Kutumia kanuni za Biblia kulimusaidia namna gani Joe na familia yake?
Marafiki wa Ana kwenye kazi, walichochea namna gani hali yake ya kiroho?
Sababu gani tuko na lazima ya ujasiri wakati wanatuchochea tutie feza pa nafasi ya kwanza katika maisha?
Namna gani Brian na Gloria walifikia kutia tena mambo ya kiroho pa nafasi ya kwanza katika maisha yao?
Ni kanuni gani za Biblia zenye ulipata katika video hii?