UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MATENDO 1-3
Roho Takatifu Inashuka juu ya Kutaniko la Kikristo
Wayahudi wengi wenye walikuwa Yerusalemu siku ya Pentekoste mu mwaka wa 33 walitoka mu inchi mbalimbali. (Mdo 2:9-11) Hata kama walikuwa wanatii Sheria ya Musa, pengine waliishi mu inchi zingine maisha yao yote. (Yer 44:1) Kwa hiyo, pengine namna ya kuona mambo na namna ya kuzungumuza ya wengi kati yao ilifanana sana na watu wa inchi yao ya kizalikio kuliko kufanana na Wayahudi. Wakati watu 3 000 kutoka inchi mbalimbali walibatizwa, mara moja kutaniko la Kikristo lilijaa watu wa aina mbalimbali. Lakini, “kila siku waliendelea kuwa katika hekalu wakiwa na kusudi moja.”—Mdo 2:46.
Namna gani ninaweza kuonyesha kama ninahangaikia kabisa . . .
watu wenye walitoka fasi ingine lakini wanaishi mu eneo yetu?
ndugu na dada wa kutaniko letu wenye walitoka fasi ingine?