UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | 2 WAKORINTO 7-10
Utumishi Wetu wa Kutoa Musaada
Utumishi wetu wa Kikristo uko na sehemu mbili. Ya kwanza ni “utumishi wa upatanisho,” ni kusema kazi yetu ya kuhubiri na kufundisha. Na ya pili ni “utumishi wa kutoa musaada” ili kusaidia waamini wenzetu. (2Ko 5:18-20; 8:4) Kwa hiyo, kusaidia Wakristo wenye wako mu uhitaji ni sehemu ya utumishi wetu mutakatifu. Wakati tunasaidia Wakristo wenzetu:
Tunatimizia ndugu na dada zetu mahitaji yao.—2Ko 9:12a
Tunasaidia wenye wamepatwa na magumu warudilie programu yao ya kiroho, ni kusema, waanze tena kujifunza kipekee, kuenda ku mikutano, na kuhubiri kwa bidii ili kumushukuru Yehova.—2Ko 9:12b
Tunamutukuza Yehova. (2Ko 9:13) Kazi ya kutoa musaada inasaidia watu wakuwe na mawazo ya muzuri juu yetu, hata wale wenye wako na mawazo ya mubaya juu ya Mashahidi wa Yehova