UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | WAKOLOSAI 1-4
Muvue Utu wa Zamani, na Muvae Utu Mupya
Wakati uligeuka na kuwa Shahidi wa Yehova, je, ilikuomba kufanya mabadiliko ya mingi? Kama ni vile, ujue kama Yehova alifurahia mabadiliko yenye ulifanya. (Eze 33:11) Lakini, inaomba uendelee kuwa muangalifu juu uendelee kuvaa utu mupya na usirudilie tena tabia za zamani. Jiulize hii maulizo juu uone fasi kwenye inaomba utengeneze:
Ningali nawekea kinyongo mutu fulani mwenye alinikoseaka?
Ninaonyeshaka uvumilivu, hata wakati niko na mambo mingi ya kufanya ao wakati nilishachoka?
Kama akili yangu inaanza kufikiria mambo ya mubaya, ninajikazaka mara moja kuacha kuifikiria?
Ninakuwaka na mawazo fulani ya mubaya juu ya watu wa kabila ao inchi ingine?
Mu siku fulani zenye zilipita, kuko siku yenye nilijibia mutu fulani kwa ukali ao kukasirika haraka?