UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | UFUNUO 10-12
‘Mashahidi Wawili’ Wanauawa na Kufufuliwa
‘Mashahidi wawili’: Ni kikundi kidogo cha ndugu watiwa-mafuta wenye walikuwa wanasimamia kazi wakati Ufalme wa Mungu ulisimamishwa mu mwaka wa 1914
Wanauawa: Kisha kuhubiri kwa miaka tatu na nusu wakiwa wamevaa “nguo za magunia,” ‘waliuawa’ wakati walifungwa na kulazimishwa kuwa mu hali ya kutotenda
Kufufuliwa: Ku mwisho wa zile siku tatu na nusu za mufano, walifufuliwa wakati waliachiliwa kutoka katika gereza na wakaanza tena kusimamia kazi ya kuhubiri