UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MWANZO 12-14
Agano Lenye Linakuhusu
Yehova alifanya agano pamoja na Abrahamu, lenye lilifanya Ufalme wa mbinguni ukuwe na musingi wa kisheria
Kwa kweli ile agano ilianza kutumika mu mwaka wa 1943 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu, wakati Abrahamu alivuka Muto Efrati katika safari yake ya kuenda Kanaani
Ile agano itaendelea kufanya kazi mupaka wakati Ufalme wa Masiya utaharibu maadui wote wa Mungu na kuletea baraka familia zote za dunia
Yehova alimubariki Abrahamu sababu alikuwa na imani sana. Kama tunaamini ahadi za Mungu, tutapata baraka gani zenye zitatokana na agano lenye Mungu alifanya pamoja na Abrahamu?