UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | KUTOKA 29-30
Kumutolea Yehova Muchango
Wakati wa kujenga tabenakulo, watu wote, ikuwe masikini ao matajiri walikuwa na pendeleo ya kutoa michango juu ya kutegemeza ibada ya Yehova. Namna gani tunaweza kumutolea Yehova muchango leo? Tunaweza kufanya vile kwa kutoa feza ili kutegemeza kazi ya kujenga Majumba ya Ufalme, Majumba ya Mikusanyiko, biro za kutafsiri, majengo mbalimbali ya Beteli, na majengo ingine yenye inatumiwa kwa ajili ya mambo ya Ufalme.
Hii maandiko inaweza kutufundisha nini juu ya kutoa michango ili kutegemeza ibada ya kweli?