UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MAMBO YA WALAWI 16-17
Siku ya Kufunika Zambi Inakufundisha Nini?
Uvumba wenye ulikuwa unatumiwa Siku ya Kufunika Zambi unaweza kutufundisha nini?
Sala za watumishi waaminifu wa Yehova ziko kama uvumba. (Zb 141:2) Kuhani mukubwa alikuwa analeta uvumba mbele ya Yehova kwa heshima kubwa; na siye pia wakati tunamukaribia Yehova katika sala, tunafanya vile kwa heshima kubwa
Kuhani mukubwa alipaswa kuchoma kwanza uvumba mbele atoe zabihu. Vilevile, mbele Yesu atoe uzima wake kuwa zabihu, alipaswa kumutii Yehova kwa ushikamanifu maisha yake yote ku dunia ili Yehova akubali zabihu yake
Naweza kufanya nini ili Yehova akubali zabihu zenye ninamutolea?