Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • mwb21 Mwezi wa 1 uku. 3
  • Wazazi, Musaidie Watoto Wenu ili Wakuwe na Ujuzi

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Wazazi, Musaidie Watoto Wenu ili Wakuwe na Ujuzi
  • Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2021
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Unaweza Kufanya Nini Juu Familia Yako Ikuwe na Furaha?​—Sehemu ya 2
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
  • Wazazi, Musaidie Watoto Wenu Wamupende Yehova
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2022
  • Wazazi, Mufundishe Watoto Wenu Wamupende Yehova
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2019
  • Wazazi, Musaidie Watoto Wenu Wakuwe na Imani Yenye Nguvu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2016
Ona Habari Zaidi
Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2021
mwb21 Mwezi wa 1 uku. 3
Wazazi wako wanafundisha watoto wao namna ya kujilinda. Wakati wa mazoezi watoto wanafanya alama ya kusema ‘Hapana!’

MAISHA YA MUKRISTO

Wazazi, Musaidie Watoto Wenu ili Wakuwe na Ujuzi

Watu fulani mu hii dunia wanasema kama wema ni ubaya na ubaya ni wema. (Isa 5:20) Na inahuzunisha kuona kama watu fulani wako wanafanya mambo yenye Yehova anachukia, sawa vile mwenendo mubaya kati ya mwanaume na mwanaume ao mwanamuke na mwanamuke. Ku masomo, vijana ao watu wengine wanaweza kuchochea vijana wetu wafuate mwenendo wao. Unaweza kufanya nini ili kutayarisha watoto wako wapambane muzuri na ile majaribu ao majaribu ingine?

Saidia watoto wako wajue kanuni za Yehova. (Law 18:3) Kulingana na miaka yao, uwafundishe hatua kwa hatua mambo yenye Biblia inafundisha kuhusu ngono. (Kum 6:7) Ujiulize: ‘Nilishafundisha watoto wangu njia ya muzuri ya kuonyesha upendo, juu ya nini ni muzuri kuvaa kwa kiasi, na juu ya nini wengine wanapaswa kuheshimia mambo yao ya kipekee? Watoto wangu wanajua kile wanaweza kufanya kama mutu fulani anapenda kuwaonyesha pornografia ao anawaambia wafanye jambo fulani lenye Yehova anakataza?’ Mambo yenye walishajua inaweza kuwasaidia waepuke hatari. (Mez 27:12; Muh 7:12) Watoto ni uriti kutoka kwa Yehova. Wakati unawafundisha, unaonyesha kama unawapenda.​—Zb 127:3.

MUANGALIE VIDEO JENGA NYUMBA YENYE HAITABOMOKA​—LINDA WATOTO WAKO ILI WASIPATWE NA “YALIYO MAOVU,” KISHA MUJIBIE HII MAULIZO:

  • Picha yenye inatoka mu video ‘Jenga Nyumba Yenye Haitabomoka​—Linda Watoto Wako ili Wasipatwe na ‘Yaliyo Maovu.’’ Mama na mutoto wake mwanaume wako wanaangalia video ‘Linda Watoto Wako.’

    Juu ya nini wazazi fulani wanajizuiaka kufundisha watoto wao kuhusu ngono?

  • Picha yenye inatoka mu video ‘Jenga Nyumba Yenye Haitabomoka​—Linda Watoto Wako ili Wasipatwe na ‘Yaliyo Maovu.’’ Wazazi wako wanazungumuza na watoto wao wawili mu kitabu ‘Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu’ na mu vichapo vingine.

    Juu ya nini wazazi wanapaswa kulea watoto wao katika “nizamu na maonyo ya Yehova”?​—Efe 6:4

  • Picha yenye inatoka mu video ‘Jenga Nyumba Yenye Haitabomoka​—Linda Watoto Wako ili Wasipatwe na ‘Yaliyo Maovu.’’ Wazazi wenye kuwa mu Afrika wako wanasoma na kuzungumuzia maandiko fulani pamoja na watoto wao.

    Ujuzi ni ulinzi

    Ni mambo gani yenye tengenezo la Yehova limepatia wazazi yenye inaweza kuwasaidia wafundishe watoto wao kuhusu ngono?​—w19.05 uku. 12, kisanduku

  • Juu ya nini unapaswa kuzungumuza na watoto wako kwa ukawaida mbele magumu itokee?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine