MAISHA YA MUKRISTO
Wazazi, Musaidie Watoto Wenu ili Wakuwe na Ujuzi
Watu fulani mu hii dunia wanasema kama wema ni ubaya na ubaya ni wema. (Isa 5:20) Na inahuzunisha kuona kama watu fulani wako wanafanya mambo yenye Yehova anachukia, sawa vile mwenendo mubaya kati ya mwanaume na mwanaume ao mwanamuke na mwanamuke. Ku masomo, vijana ao watu wengine wanaweza kuchochea vijana wetu wafuate mwenendo wao. Unaweza kufanya nini ili kutayarisha watoto wako wapambane muzuri na ile majaribu ao majaribu ingine?
Saidia watoto wako wajue kanuni za Yehova. (Law 18:3) Kulingana na miaka yao, uwafundishe hatua kwa hatua mambo yenye Biblia inafundisha kuhusu ngono. (Kum 6:7) Ujiulize: ‘Nilishafundisha watoto wangu njia ya muzuri ya kuonyesha upendo, juu ya nini ni muzuri kuvaa kwa kiasi, na juu ya nini wengine wanapaswa kuheshimia mambo yao ya kipekee? Watoto wangu wanajua kile wanaweza kufanya kama mutu fulani anapenda kuwaonyesha pornografia ao anawaambia wafanye jambo fulani lenye Yehova anakataza?’ Mambo yenye walishajua inaweza kuwasaidia waepuke hatari. (Mez 27:12; Muh 7:12) Watoto ni uriti kutoka kwa Yehova. Wakati unawafundisha, unaonyesha kama unawapenda.—Zb 127:3.
MUANGALIE VIDEO JENGA NYUMBA YENYE HAITABOMOKA—LINDA WATOTO WAKO ILI WASIPATWE NA “YALIYO MAOVU,” KISHA MUJIBIE HII MAULIZO:
Juu ya nini wazazi fulani wanajizuiaka kufundisha watoto wao kuhusu ngono?
Juu ya nini wazazi wanapaswa kulea watoto wao katika “nizamu na maonyo ya Yehova”?—Efe 6:4
Ujuzi ni ulinzi
Ni mambo gani yenye tengenezo la Yehova limepatia wazazi yenye inaweza kuwasaidia wafundishe watoto wao kuhusu ngono?—w19.05 uku. 12, kisanduku
Juu ya nini unapaswa kuzungumuza na watoto wako kwa ukawaida mbele magumu itokee?