TUJITOE KABISA KATIKA KAZI YA KUHUBIRI | ONGEZA FURAHA YAKO MU KAZI YA KUHUBIRI
Tumia Mifano ili Kukazia Mawazo Makubwa
Wakati tuko narudilia watu ao kuongoza mafunzo ya Biblia, tunapaswa kujikaza kuwasaidia waelewe mawazo makubwa. Kwa kutumia mifano ili kukazia ile mawazo, tunaweza kuchochea mioyo yao na kufanya ikuwe mwepesi kwao kukumbuka mambo yenye wako najifunza.
Wakati uko najitayarisha ili kurudilia mutu ao kuongoza funzo la Biblia, tafuta mawazo makubwa na utayarishe mifano ili kuikazia; hapana kukazia mambo ya kidogo-kidogo. Ni muzuri kutayarisha mifano ya mambo ya kawaida mu maisha ya watu. (Mt 5:14-16; Mk 2:21; Lu 14:7-11) Fikiria maisha ya musikilizaji na kazi yenye anafanyaka. (Lu 5:2-11; Yoh 4:7-15) Wakati unaona anafurahi juu anaelewa wazo fulani, na weye utafurahi.
MUANGALIE VIDEO PATA FURAHA KATIKA KAZI YA KUFANYA WANAFUNZI—KOMALISHA UFUNDI WAKO—KWA KUTUMIA MIFANO ILI KUKAZIA MAWAZO MAKUBWA, KISHA MUJIBIE HII MAULIZO:
Juu ya nini wanafunzi wanaweza kuwa na lazima ya kusaidiwa ili waelewe Maandiko fulani yenye kuwa mu Biblia?
Neeta alitumia mufano gani ili kufasiria kweli yenye kuwa mu Waroma 5:12?
Mifano ya muzuri inagusaka moyo
Namna gani mifano ya muzuri inaweza kusaidia wasikilizaji wetu?
Juu ya nini wakati tuko mu mahubiri, tunapaswa kutumia video na vyombo vingine vya kufundishia vyenye tuko navyo mu tengenezo la Yehova?