MAISHA YA MUKRISTO
Tendea Wanamuke Wenye Kukomaa Kama Mama, na Vijana Wanamuke Kama Dada
Maandiko inatuomba tutendee Wakristo wenye kuzeeka sawa vile tunatendeaka mama na baba yetu, na tutendee vijana Wakristo sawa vile tunatendeaka ndugu na dada zetu wenye tunazaliwa nao. (Soma 1 Timoteo 5:1, 2.) Zaidi sana ndugu wanapaswa kutendea dada kwa heshima.
Ndugu hapaswe hata kidogo kuchezea dada kimapenzi ao kufanya jambo fulani yenye inaweza kumufanya dada akuwe najisikia mubaya wakati iko karibu yake. (Yob 31:1) Ndugu mwenye hayaoa, hapaswe kucheza na hisia za dada mwenye hayaolewa kwa kumufanya ajisikie kama anapendezwa naye kimapenzi, kumbe haiko vile.
Wakati dada wanauliza kwa heshima wazee ulizo fulani ao hata wakati wanatoa mawazo fulani yenye inaomba kufikiria sana, wazee wanapaswa kuwahangaikia. Zaidi sana wazee, wanapaswa kuhangaikia bibi wenye hawana bwana wa kuwalinda.—Rut 2:8, 9.
MUANGALIE VIDEO ONYESHA UPENDO WA KWELI KATIKA KUTANIKO—KWA WAJANE NA WATOTO WENYE HAWANA BABA, KISHA MUJIBIE HII MAULIZO:
Ndugu na dada walifanya nini ili kuonyesha upendo wa kweli Dada Myint?
Upendo wenye ndugu na dada walionyesha, ulikuwa na matokeo gani juu ya watu wa mu kijiji?
Upendo wenye ndugu na dada walionyesha, ulichochea watoto wanamuke wa Dada Myint wafanye nini?
Unaweza kufanya nini ili kuonyesha kama unahangaikia kwa upendo dada wa mu kutaniko yako?